• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Wanawake waaswa kupima Saratani za Matiti na Mlango wa Kizazi

Posted on: April 23rd, 2018

Wanawake nchini wameaswa kuwa na tabia ya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara wa Saratani za matiti na mlango wa kizazi ili kupata tiba mapema iwapo watagundulika kuwa na virusi vya Saratani hizo.

Wosia huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack wakati akizindua zoezi la utoaji chanjo mpya ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wa miaka 14 mapema leo katika eneo la Nguzo nane, Manispaa ya Shinyanga. 

Katika hotuba yake ya uzinduzi Mhe. Telack amesema Saratani ya mlango wa kizazi ndiyo inayoongoza kusababisha vifo kwa wanawake kuliko saratani nyingine ndiyo sababu Serikali imeamua kutoa chanjo hii. 

" Kwa mwaka, takribani wanawake 4000 wanafariki kwa sababu ya saratani hii" amesema Telack. 

Aidha, amewataka wanawake kuwahi kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya iwapo wataona dalili zozote za ugonjwa wa saratani.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Josephine Matiro amesema, Wilaya ya Shinyanga imetoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kupitia viongozi na watendaji wa ngazi zote ili wananchi wote waelewe umuhimu wa chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi na wote wananostahili kupata chanjo wafikiwe.

Awali, Katibu Tawala Msaidizi Afya katika Sekretarieti ya Mkoa Dkt. Rashid Mfaume amesema kuwa, uzinduzi wa chanjo ya saratani hii unafanyika nchi nzima ambapo wasichana wote wenye umri wa miaka 14 watapata chanjo hii.

Dkt. Rashid ameongeza kuwa, kuanzia mwaka ujao wasichana watakaopata chanjo hiyo ni wa miaka 9 - 14 na baadaye itakuwa inafanyika kila mwaka kwa wasichana wa miaka 9 lengo likiwa ni kuwazuia wasichana ambao hawajaanza kujihusisha na ngono kupata virusi vinavyosababisha Saratani hiyo.

Saratani za matiti na mlango wa Kizazi zinaelezwa kuongoza kuathiri wanawake hasa katika nchi zinazoendelea ambapo saratani ya mlango wa kizazi ndiyo inayoongoza kwa kusababisha vifo. 

Wanawake 466,000 kila mwaka duniani wanagundulika kuwa na Saratani hii wakati nchini Tanzania wanawake 7304 wanaugua na kati ya hao 4,216 sawa na asilimia 58 hufariki.

Kwa Mkoa wa Shinyanga, wasichana walengwa wa kupata chanjo hiyo ni zaidi ya elfu 29.

Matangazo

  • Matokeo ya kidato cha nne na QT 2018 January 24, 2019
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga August 17, 2018
  • Uzinduzi wa Utoaji wa Chanjo mpya ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi April 20, 2018
  • Ziara ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mkoani Shinyanga July 05, 2018
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Matukio katika picha, ziara ya Mhe. Balozi Seif Ally Iddi Mkoani Shinyanga

    February 13, 2019
  • Shinyanga yapata magari yenye thamani ya sh. mil 189 kwa ajili ya shughuli za UKIMWI

    February 07, 2019
  • Ofisi za RC na DC zisiwe mahakama

    February 02, 2019
  • Wadau watoe elimu kuwazuia vijana kufanya ngono, siyo matumizi ya kondomu

    February 01, 2019
  • Angalia zote

Video

MAKABIDHIANO YA MWENGE WA UHURU 2018 MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Hati ya Mshahara

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa