• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

ANDIKENI TAARIFA ZENYE AJENDA ZA KITAIFA

Posted on: May 29th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) amewataka waandishi wa habari Mkoani Shinyanga kuandika habari zenye Ajenda za Kitaifa ikiwamo ujenzi wa Miundombinu mbalimbali miradi mikubwa ya kimkakati pamoja na kuhabarisha umma juu ya uwepo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu wa 2024 sanjari na hatua ambazo zinaendelea kutekelezwa ikiwamo uboreshaji wa daftari la wapiga kura.

DC Mtatiro ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ameyasema haya leo tarehe 29 Mei, 2024 katika Semina iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (SPC) na Umoja wa Klabu za Habari Tanzania (UTPC) katika ukumbi wa mikutano uliopo Karena Hotel hapa Manispaa ya Shinyanga huku akiwaahidi ushirikiano wakati wote na kwamba katika uongozi wake hapa hatokubali kuona mwanahabari akibughuziwa katika utekelezaji wa majukumu yake

"Pamoja na kuwapongeza sana Wanahabari Mkoa wa Shinyanga (SPC) kwa kushirikiana na Umoja wa Klabu ya Habari Tanzania (UTPC) kwa Semina hii nzuri ya Kijamii kuhusu Uhuru wa Kujieleza, lakini niwatake sasa kwenda kuandika habari zinazobeba Ajenda za Kitaifa ili umma uweze kuelewa," amesema DC Mtatiro.

Aidha, DC Mtatiro amesisitiza kwamba katika uhuru huo wa kujieleza unaotajwa basi uendane na mipaka sanjari na kuzingatia Sheria za nchi kwakuwa hakuna yeyote aliye juu ya sheria, na ili kukwepa kuingia kwenye mikono ya sheria, waandishi wanapaswa kuchakata habari zao kwa ufasaha na ziwe na uwiano wa pande zote mbili.

Akisoma risala  kwa mgeni rasmi, Mwenyekiti wa SPC Bw. Greyson Kakuru amesema kuwa dhumuni la Semina hii ni kujadili kwa pamoja juu ya hali ya uhuru wa kujieleza kwa muktadha wa kusukuma na kuchochea maendeleo kwa sekta zote, ili kuona umuhimu wa uhuru wa kujieleza unavyoleta tija ya maendeleo hapa nchini.

Ndani ya Semina hii pia Mada mbalimbali zimejadiliwa ikiwamo ya Uhuru wa kujieleza, Utawala Bora kwa Maendeleo ya Mkoa wa Shinyanga, na Umuhimu wa upatikanaji wa Taarifa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa