• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

BI. DAFROZA NDALICHAKO AFUNGUA MAFUNZO WA SHINYANGA YA NeST MKOA WA SHINYANYA

Posted on: August 28th, 2023

Na. Shinyanga RS.

KATIBU Tawala Msaidizi (ELIMU) Mkoa wa Shinyanga Bi. Dafroza Ndalichako ambaye alimuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo amefungua mafunzo ya mfumo mpya wa ununuzi NeST kwa wataalam 36 kutoka katika Halmashauri zote 6 zinazounda Mkoa wa Shinyanga huku akiwataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote ndani ya Mkoa wa Shinyanga kusimamia na kutekeleza kwa weledi matumizi ya Mfumo huu mpya.

Bi. Ndalichako amewaeleza watalaam hao ambao walionesha utulivu na umakini wakati wote kuwa ujio wa mfumo huu mpya wa ununuzi unakwenda kuwa mwarobaini wa hujuma zilizokuwa zikijitokeza katika ununuzi na kuondoa kabisa urasimu ambao awali ulikuwa ukijitokeza huku akiwaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga kwenda kusimamia na kutekeleza kwa weledi mfumo huu katika maeneo yao ili tija ya mfumo huu iweze kuonekana.

"Nawaagiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri zetu zote 6 kwenda kusimamia na kutekeleza mfumo huu mpya ili uweze kuwa na tija kama ambavyo Serikali imekusudia," alisema Bi. Ndalichako.

Kando na maelekezo hayo, lakini pia Bi. Ndalichako aliishukuru sana Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazozifanya, pia aliwapongeza sana na kutambua mchango wa Mtendaji Mkuu (PPRA) Ndg. Joackim Maswi na Mamlaka yenyewe kwa kufadhiri na kufanikisha mafunzo haya ambayo yameanza leo hii tarehe 28 Agosti, 2023 katika ukumbi wa mikutano hapa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na yatafikia tamati tarehe 1 Sept, 2023.

PPRA walitoa mafunzo kama haya kwa maafisa kutoka Sekretarieti za Mikoa ya Tanzania Bara  Jijini Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuutumia mfumo ili na wao waweze kuwafundisha waliopo katika ngazi za Halmashauri ili nao wakawafundishe walipo katika maeneo yao ya kazi.

Picha ikionesha baadhi ya wakufunzi na wataalam wakiwa katika mafunzo ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa