• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Bil 2.6 kufanya mapinduzi ya Vituo sita vya Afya Mkoani Shinyanga

Posted on: January 18th, 2018

Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara ya Afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto, Wizara ya fedha na mipango na wadau wa maendeleo imetoa jumla ya sh. Bil 2.6 kwa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kujenga na kukarabati vituo vya Afya 6 ili vituo hivyo viweze kutoa huduma za dharura za uzazi ikiwemo upasuaji.

Akizungumza katika ziara ya ufuatiliaji wa ukarabati wa vituo hivyo,Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya huduma za Ustawi wa jamii kutoka OR-TAMISEMI bw. Rasheed Maftaha ambaye anaongoza timu hiyo ya ufuatiliaji, amesema kuwa Serikali imeweka mkakati madhubuti wa kuimarisha vituo vya Afya 513 nchi nzima ili viweze kutoa huduma za dharura.

Maftaha amesema Serikali imeshapeleka fedha katika vituo 44 nchi nzima ambavyo vipo katika hatua ya ukamilishaji.

Aidha, vituo vingine 139 nchini vimeshapelekewa fedha kwa ajili ya kuanza ukarabati mara moja.

Mkoa wa Shinyanga umepata sh. 2.6 bil katika vituo vya Afya 6 ambavyo ni Songwa katika Wilaya ya Kishapu kilichopata sh. Mil 400.

Katika Wilaya ya Shinyanga vituo viwili vimepokea jumla ya sh. Mil 900 ambavyo ni Samuye sh. Mil 500 na Tinde sh. Mil 400, katika Wilaya ya Kahama kituo cha Chela kimepokea sh. Mil 400, Iyenze sh. Mil 500 pamoja na Ukune sh. Mil 400.

Katika awamu ya kwanza iliyotolewa mwezi Agosti mwaka jana 2017, kituo cha Afya Iyenze kilichopo Halmashauri ya Mji Kahama kipo katika hatua ya ukamilishaji, ambapo vituo vingine vya Songwa, Samuye, Tinde, Chela na Ukune vimeshaanza maandalizi ikiwemo kutenga maeneo ya ujenzi pamoja na uundaji wa kamati za kusimamia ujenzi huo kutoka kwenye uwakilishi wa wananchi.

Maftaha amesema mkakati huo wa sh. 1.3 trilioni unafadhiliwa na Benki ya dunia, Serikali ya Canada pamoja na Serikali ya Denmark ni muendelezo wa utekelezaji wa mpango wa MMAM ambao kwa miaka 10 umekuwa haujatekelezwa kikamilifu.

Timu hiyo ya ufuatiliaji ipo Mkoani Shinyanga kwa siku 3 na imetembelea Wilaya zote tatu za Shinyanga, Kishapu na Kahama, kuona utekelezaji wa ukarabati wa vituo hivyo.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa