• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

BIL.9 KUIJENGEA UWEZO MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA SHINYANGA (SHUWASA)

Posted on: November 4th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKURUGENZI Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) Mhandisi Yusuph Katopola amesema takribani shilingi Bilioni 9 zitatumika kuijengea uwezo Taasisi, Watumishi na sehemu zingine katika kuboresha na kutoa huduma za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa wananchi Mkoani Shinyanga.

Ameyasema haya leo tarehe 4 Novemba, 2024 wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa miaka 4 wa kuijengea Taasisi uwezo baina yake na Mhandisi Mshauri wa Kampuni ya Gopa Infra ya Ujerumani ikishirikiana na Kampuni ya Superlit Consulting Ltd ya Tanzania, hafla ambayo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo makao makuu ya SHUWASA Manispaa ya Shinyanga.

“Kupitia Mkataba huu ambao tumesaini leo na Kampuni ya Gopa Infra naamini unakwenda kutimiza jukumu kubwa la kuijengea uwezo Taasisi yetu, watumishi na sehemu zingine ili kutekeleza uboreshaji na utoaji wa huduma za Majisafi na usafi wa Mazingira katika mkoa wetu wa Shinyanga” amesema Mha. Katopola.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa Kampuni ya Gopa Infra Stefan Doerner, amefurahi kupata fursa ya kufanya kazi nchini huku akiahidi kuisaidia kuijengea uwezo SHUWASA ili kuhakikisha wanatoa huduma bora za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa wananchi.

Mkataba huu ambao ni wa miaka 4 ni sehemu mojawapo ya mradi mkubwa wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye thamani ya Euro Milioni 76 ili kuwafikia wananchi wengi wapate huduma ya maji.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa