• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Bodi mpya ya Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga yazinduliwa

Posted on: May 18th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amewataka wajumbe wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga kutumia taaluma na uzoefu wao kusaidia uongozi wa Hospitali kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga.

Akizindua Bodi hiyo mpya itakayodumu hadi tarehe 31/04/2019, Mhe. Telack amewaambia wajumbe hao kuwa wameaminiwa na kuteuliwa kuwakilisha wananchi katika kufanya maamuzi ya Hospitali ya Mkoa, hivyo hategemei watafanya kwa maslahi yao binafsi kinyume na malengo yaliyokusudiwa.

"Bodi ya ushauri ya hospitali ya rufaa ya Mkoa ni chombo muhimu sana katika uendeshaji wa huduma za afya za hospitali za mikoa. Hiki ndicho chombo pekee kinachowaunganisha wananchi na Serikali yao katika ngazi ya hospitali ya rufaa ya Mkoa. Ni chombo ambacho kina wawakilisha wananchi katika kufanya maamuzi juu ya utoaji wa huduma katika hospitali ya rufaa ya Mkoa. Bodi inaweza kufananishwa na kioo ambacho menejimenti ya hospitali inakitumia kupata mrejesho wa namna wanavyotoa huduma kwa wananchi". amesema Mhe. Telack.

Mhe. Telack amesema, kazi kubwa ya Bodi ni kuishauri menejimenti ya hospitali na mamlaka zingine kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa kufuata Miongozo, Sheria, Kanuni na Taratibu za Nchi. 

Ametoa angalizo kuwa, Serikali inahitaji bodi inayofanya kazi kwa ubunifu na kwa kujitolea. Sio bodi inayofanya kazi kwa kutegemea uwepo wa posho. "Kuna baadhi ya wajumbe wa bodi wa awamu zilizopita walikuwa wanagoma kuja kwenye vikao mpaka fedha za kuwalipa posho zitakapopatikana. Wajumbe wa namna hiyo kama wapo kwenye bodi hii basi ni vema wabadilishe mitazamo yao". 

Aidha, Telack ameitaka bodi kuisaidia hospitali ili iweze kupata fedha zitakazosaidia kuendesha hospitali na kuibua fursa mbalimbali zitakazoboresha upatikanaji wa huduma bora na kuwa Serikali haitasita kuivunja bodi hiyo iwapo itashindwa kufanya kazi.

"Kwa kweli, Sisi upande wa Serikali hatutasita kuivunja bodi hii kama itashindwa kufanya kazi zake au itakuwa mzigo kwa hospitali kinyume na matarajio yetu".

Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa Bw. Alfred Shayo amesema kuwa anaamini bodi hiyo itasaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa watumishi, madeni ya wazabuni na watumishi pamoja na uchakavu wa miundombinu. 

Bw. Shayo amesema pia kuwa, Serikali ipo tayari kushirikiana na bodi na kupokea ushauri utakaotolewa kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wananchi.

Akitoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa kuzindua bodi hiyo, Mwenyekiti wa bodi Dkt. Ernest Haraka amesema bodi itajitahidi kutafuta suluhisho kwa changamoto zilizopo ikiwemo suala la watumishi na kutafuta mapato ili waweze kuwasaidia wananchi kwa njia yoyote ile kupitia wadau mbalimbali.

Dkt. Haraka ameahidi pia kuwa watazingatia yote waliyoelekezwa kwa kuyafanyia kazi jinsi ilivyokusudiwa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa