#shinyanga_rs
BODI ya Parole Mkoa wa Shinyanga imeitaka Serikali kuongeza juhudi ya utoaji wa elimu zaidi kwa jamii kuhusu maadili, malezi na makuzi ilimkuweza kuwa na jamii bora na yenye hofu ya Mungu jambo ambalo litapelekea kupunguza uhalifu na msongamano Magerezani.
Bodi iliongozwa na Mwenyekiti Bi. Zipporah Lyon Pangani, Kaimu Katibu wa Parole Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP) Hilary Cafmir Kimbi, Afisa Parole wa Mkoa Shinyanga, Mkaguzi wa Magereza(INSP) Winston Juma Leonard, pamoja na wajumbe wengine ambao ni Mwendesha Mashtaka Mkoa, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa, Mwanasheria na Wakili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dinnah Kiganga, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Yudas Ndungile, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa Bi. Lydia Kwesigabo na wajumbe wengine wa Bodi ya Parole wa kuteuliwa na Waziri wa Mambo ya Ndani.
Kwa ujumla, Bodi ya Parole ilifanya ziara tarehe 29 na 30 Aprili 2025 katika gereza la Wilaya la Kahama na hinyanga Lengo la ziara lilikuwa ni kukutana na wafungwa pamoja na mahabusu ili kutoa elimu mbalimbali ikiwemo uwepo wa bodi hiyo na majukumu yake pamoja na kupata maoni mbalimbali toka kwao.
Boma Street, Mwanza Road
Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga
Simu: +255 28 2762222
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz
Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa