• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

DC MBONI MHITA AIPONGEZA MSALALA

Posted on: August 24th, 2023

Na Shinyanga RC.

MKUU Wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita ameipongeza Halmashauri ya Msalala kwa jitihada zake mbalimbali zinazofanywa zikiwa na lengo la kutimiza ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) lengo likiwa ni kuleta maendeleo kwa Wilaya na taifa kwa ujumla.

Pongezi hizo zimetolewa leo katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Msalala wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Waheshimiwa Madiwani na wakuu Divisheni na Vitengo wa Msalala ambapo pia amemshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme kwa kukubali ombi la kutoa wakufunzi wawili kuwezesha mafunzo hayo.

Mafunzo haya ni yenye kuongeza ufanisi katika kusimamia miradi ya maendeleo ndani ya mamlaka wanazoziongoza kwani Mheshimiwa Diwani ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Kata na ikumbukwe Serikali ya awamu ya sita inapeleka fedha nyingi Katani hivyo mafunzo haya yataongeza maarifa zaidi katika kusimamia miradi hiyo.

Kwa upande wao Waheshimiwa Madiwani wamemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi ndani ya Halmashauri Ili kuhakikisha jamii inaimarika kwa kuwa na huduma za msingi ikiwemo Afya, Elimu, Maji, Barabara na Nishati ya Umeme vijijini kupitia mradi wa REA na kumwomba Mkuu wa Wilaya Mhe. Mboni Mhita kufikisha salamu za Baraza kwa Mhe. Rais na kuahidi kusimamia miradi yote kwa ufasaha.

Sambamba na hilo Baraza limewapongeza Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Mibako Mabubu na Mkurugenzi Mtendaji (W) ndg. Khamis Katimba kwa kuwezesha mafunzo haya ambayo yamelenga viongozi hawa kujua mipango ya bajeti Halmashauri inayopanga na hivyo kuwa rahisi kwao kufanya ufuatiliaji katika ngazi mbalimbali ikiwemo Halmashauri na Serikali Kuu.

Nae Katibu Tawala (W) ndg. Mohamed Mbega amewataka viongozi hao kufanya kazi zao kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni ili kulinda heshima na maadili ya uongozi.

Kwa upande wao Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) wamewaomba viongozi hao kutoa ushirikiano Kwa maafisa wa Taasisi hiyo kwani wana mpango wa kutembelea Kata zote kwa ajili ya kuanzisha Huduma ya Takukuru Rafiki yenye lengo la kuongeza uwajibikaji na utoaji huduma bora kwa jamii na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi moja kwa moja.

Sehemu ya muonekano wa wajujbe wa mafunzo wakiwa ukumbini

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa