• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

Posted on: June 5th, 2021

DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati amesema Mkoa wa Shinyanga ni Mkoa wenye utajiri wa rasilimali lakini hali ya maisha ya wananchi Mkoani humo haiendani rasilimali zilizopo katika mkoa huo akiitaja hiyo kuwa changamoto kubwa ya mkoa wa Shinyanga.

Dkt. Sengati amesema hayo leo wakati wakati wa kumkaribisha Katibu Tawala Mpya wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Batlida Buriani ambaye kwa mara ya kwanza amefika katika ofisi yake mpya tayari kwa makabidhiano ya ofisi na kuendelea majukumu yake mapya.

Dkt. Sengati aliongeza kuwa Shinyanga kuna umasikini ambao umejificha katika utajili mkubwa lakini hususani kwa wakazi wa pembezoni akihaidi kuifanyia kazi changamoto hiyo ili wakazia wa mkoa wa Shinyanga waweze kuinua hali yao itakayoendana na rasilinmali zilizopo.

‘’Unakuta mtu ana ngombe zaidi ya elfu moja lakini mtu huyo anaishi katika mazingira yaliyoduni sana au haoni faida ya kupeleka mtoto katika elimu ya juu hii changamoto ambayo lazima tuifanyie kazi”. Alisisitiza Dr. Philemon Sengati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Dkt. Batlida Buriani amesema kuwa lazima kuwe na ubunifu katika kutafuta vyanzo vipya vya mapato na kuzitaka Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga kukusanya mapato bila ya kuleta kero kwa wananchi.

Aidha Dkt. Buriani amesema pia ipo aja ya kuingalia upya mianya yote ambayo imekuwa ikichangia upoteaji wa mapato kwa lengo la kuinua na kukuza uchumi wa mkoa wa Shinyanga.

Pamoja na mambo mengine Dkt.Buriani amesema ataliangazia pia sula la maendeleo na ustawi wa jamii kwa kuhakikisha ipo miradi ambayo inaweze kuingiza kipato kwa wazee na wanawake ili nao waweze kuchangia katika kujiletea maendeleo lakini pia kuchangia katika maendeleo ya Taifa.

‘’Najua Shinyanga kuna wazee wengi sana na hali zao sio nzuri na katika jambo ambalo ninataka tufanikiwe ni kuhakikisha wanashiriki katika miradi ambayo itawanufaisha najua kuwa Shinyanga kuna mifugo mingi hivyo tunaweza tukatumia fursa ya mifugo iliyopo kuzalisha siagi kwa wingi sana.’’Alisema Dkt. Batlida Buriani Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga.

Naye aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Albert Msovera alisema Mkoa wa Shinyanga bado una chanagamoto ya watumishi lakini zipo juhudi ambazo zimekuwa zikiendelea kuhakikisha changamoto hiyo inatatuliwa na hivyo kumtaka mrithi wake kuangalia namna bora ya kuendelea kulifanyia kazi jambo hilo ili kukabiliana na upungufu wa rasilimali watu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa