• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

GAKI AMELETA MAPINDUZI MAKUBWA KATIKA ZAO LA PAMBA - BASHE

Posted on: September 12th, 2024

Na Paul Kasembo, SHY RS.

WAZIRI wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (MB) amempongeza Mkurugenzi wa Gaki Investment Co. LTD ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanunuzi wa Pamba Tanzania  ndg. Gasper Kileo kwa kuwa mwekezaji wa kuigwa ambaye ameleta mapinduzi makubwa katika zao la pamba huku akimtolea mfano mzuri wa utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ambaye ameajiri Maafisa Ugani Kilimo 15 wanaohudumia Kata 3 ya Kishapu, Meatu iliyopo Simiyu na Mbutu mkoani Tabora.

Mhe. Bashe ameyasema haya leo tarehe 12 Septemba, 2024 katika ziara yake ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Shinyanga ambapo pia amefika katika kiwanda kinachozalisha zao la pamba akiwa ameambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamiringi Macha ambapo pia amesisitiza kuwa Serikali inafanya jitihada kubwa katika kuhakikisha uzalishaji wa zao la pamba unaongezeka zaidi.

“GAKI Investment ni moja kati ya wadau wakubwa wa zao la pamba ambaye anashiriki kwa kiasi kikubwa katika ununuzi wa zao na kuleta mapinduzi makubwa ya viwanda vya pamba nchini, lakini pia ametekeleza maelekezo ya Serikali ya kuhakikisha wawekezaji wa bidhaa za kilimo wanaajiri Maafisa Ugani Kilimo ili waweze kuongeza tija katika Sekta ya kioimo kwani wao wamesomea na hivyo watasaidia kupitia taaluma zao” amesema Mhe. Bashe.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamiringi Macha amesema atakutana na Maafisa Ugani Kilimo wote pamoja na wadau wengine wa pamba ili kuhakikisha wanaendelea kutekekeleza maelekezo ya Serikali na kuhakikisha uzalishaji wa zao la pamba unaongezeka hatua kwa hatua.

“Katika hili, nami nitahakikisha ninakutana na Maafisa Ugani Kilimo ambao wamejiandaa vizuri wakiwa na vifaa vya kutosha tayari kwa kazi pamoja na wadau wengine wa pamba ili kuhakikisha tunatekeleza maagizo ya Serikali na kuhakikisha tunazalisha zao la pamba kwa wingi hatua kwa hatua” amesema RC Macha.

Naye Mkurugenzi wa Gaki Investment ndugu Gasper Kileo amesema wanafuata maelekezo ya Serikali kwa kutonunua pamba maeneo mengine na badala yake wananunua pamba katika maeneo waliyoelekezwa na wamefanikiwa kupata pamba ambayo imekidhi mahitaji ya msimu mzima.

“Tumejitahidi kwa kiasi kikubwa kufuata maelekezo ya serikali ya kununua pamba maeneo ambayo tumeelekezwa na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupata pamba ambayo inatusaidia kukidhi mahitaji yetu ya uzalishaji kwa msimu huu mzima” amesema Gasper.

Ikumbukwe kuwa Shinyanga ni moja kati ya Mikoa ambayo inazalisha zao la pamba hivyo kwa kufuata maelekezo ya serikali kuhusu zao hili uzalishaji wa pamba utaongezeka kwa kiasi kikubwa na utakuwa wenye tija zaidi.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa