Na. Paul Kasembo, Bulyanhulu - Kakola.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya Ukimwi Mhe. Hassan Mtenga akiwa ameongozana na wajumbe wake ameupongeza uongozi wa Mgodi wa Bulyanhulu kwa utekelezaji wa mpango wa Mgodi wa Bulyanhulu katika kudhibiti maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) na kuajiri Watanzania zaidi ya asilimia 97.
Mhe. Mtenga ameyasema hayo leo Machi 16, 2025 baada ya Kamati hiyo kuutembelea na kuukqgua mradi wa Uchimbaji Madini wa Mgodi wa Bulyanhulu uliopo Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine Kamati hiyo imeridhishwa na na mpango wa mgodi huo unavyodhibiti maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
"Sisi kama Kamati tumeridhishwa na namna mgodi unavyoendesha kazi zake maana uwepo wa mradi huu kwa njia ya uwekezaji ni sifa kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwakuwa ndiye mlezi mkuu wa mradi huu, sisi kama Kamati tumefarijika kusikia kwamba 97% ni Watanzania wameajiriwa na wanafanya kazi kwenye mgodi huu na tunatoka hapa tukiwa na imani kubwa na mradi huu" alisema Mhe. Mtenga.
Meneja wa Mgodi wa Bulyanhulu ndg. Victor Lule amesema mgodi huo pamoja na uzalishaji wake bado umeendelea kuweka kipaumbele cha afya kwa watumishi wa mgodi huo ambapo huduma za afya kama zahanati, Huduma za kwanza hupatikana kwenye Mgodi huo na kwamba mgodi umekuwa ukipambana kuhakikisha watumishi wake wanaepukana na vitendo vitakavyopelekea kupatikana kwa waathirika wa magonjwa ya kuambukiza ikiwemo VVU jambo ambalo linashughuliliwa na Kamati hiyo.
Katika hatua nyingine Naibu waziri wa Madini Dkt Steven Kiruswa kwa niaba ya Serikali amesema maelekezo yaliyotolewa na Kamati hiyo yatafanyiwa kazi kwa lengo la kuboreshaji uzalishaji kwenye mradi wa mgodi wa Bulyanhulu ambapo Serikali ndio mbia mkuu katika mradi huo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema uwepo wa Mgodi wa Bulyanhulu unayo manufaa makubwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala na hata Mkoa wa Shinyanga kwa ujumla, hivyo kitendo cha Kamati ya Afya na Maswala ya Ukimwi kutembelea mgodi huo kitarahisisha malengo yaliyowekwa na mgodi yanafikiwa ipasavyo.
Boma Street, Mwanza Road
Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga
Simu: +255 28 2762222
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz
Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa