• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Lishe Mkoa yaweka Mikakati ya kukabiliana na lishe duni

Posted on: November 23rd, 2017

Kamati ya lishe ya Mkoa wa Shinyanga imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa, Halmashauri zote zinatenga bajeti kupitia vyanzo vya mapato vya uhakika kuanzia mwaka ujao wa fedha kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa shughuli za lishe Mkoani hapa ili kukabiliana na tatizo la lishe.

Wakizungumza katika kikao cha kawaida cha kila robo mwaka, wajumbe wa Kamati hiyo inayoundwa na Wataalamu wa Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa pamoja na wadau wanaojishughulisha na huduma za lishe wamesema kuwa, moja ya sababu zinazofanya hali ya lishe kuwa mbaya Mkoani hapa ni pamoja na shughuli za lishe kutopewa kipaumbele katika mipango na bajeti.

Afisa lishe Mkoa Bw. Dennis Madeleke, akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Septemba mwaka huu, amesema kuwa hakuna shughuli ya lishe iliyotekelezwa kwa kutumia fedha za mapato ya ndani kwa kipindi hicho na kuongeza kuwa bado hali ya lishe siyo nzuri Kimkoa.

Kufuatia hali hiyo, kamati kwa pamoja imedhamiria kuhakikisha Halmashauri zote zinafuata muongozo wa Serikali wa kutenga kwenye bajeti sh. 1000 kwa mwaka kwa ajili ya utekelezaji wa huduma za lishe kwa kila mtoto wa chini ya miaka 5.

Awali akifungua kikao cha kamati hiyo, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya katika Sekretarieti ya Mkoa Dkt. Rashid Mfaume amesema kuwa changamoto bado ni kubwa hasa kwa akinamama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kuwa na upungufu wa damu ambapo amesema asilimia 59.4 ya akinamama wajawazito kwa mwaka wanakuwa na tatizo la upungufu wa damu wakati wa kujifungua hivyo kusababisha vifo. Aidha, watoto chini ya miaka mitano ni asilimia 7.

Pamoja na mkakati huo wa kutenga bajeti, kamati ya lishe pia imeazimia kuendelea kushirikiana na wadau wanaojishughulisha na huduma za lishe kwa kuhakikisha wadau hao wanatumia Wataalamu wa Serikali katika kutekeleza majukumu yao.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa