• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA SIASA MKOA WA SHINYANGA YAHITIMISHA ZIARA YA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM 2020/2025

Posted on: February 24th, 2024

Na. Shinyanga RS

KAMATI ya Siasa Mkoa wa Shinyanga imehitimisha ziara yake ya utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020/2025 katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ambapo pamoja na pongezi kwa utekelezaji mzuri wa Ilani lakini pia Kamati imeishauri Serikali kuboeresha na kuimarisha kivuko cha wananchi kuingia soko jipya la Ibinzamata.

Hayo yamebainishwa tarehe 24 Februari, 2024 na Ndugu John Siagi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga ambaye alimuwakilisha Mwenyekiti CCM Mkoa wa Shinyanga Ndugu Mabala Mlolwa ambaye alipata udhuru huku akisisitiza pia uboreshwaji wa mazingira katika Shule mpya ya Sekondari Butengwa ambapo amewataka kupanda miti ya matunda na vivuli.

Awali Kamati ilikagua utekelezaji wa Ilani katika Shule mpya ya Wasichana Shinyanga ambapo ameitaka Serikali kusimamia vema ujenzi wa majengo ili yawanufaishe na vizazi vijavyo, huku akipongeza zaidi ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharula Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga ambapo pia alisisitiza kuzingatiwa kwa uadilifu, maadili ya kazi zao na utendaji kazi bora ukizingatia kuwa wanahudumia wananchi.

"Tuipongeze Serikali kwa utekelezaji wa Ilani yetu ya CCM 2022/2025 katika sekta ambazo Kamati imekagua, na kwamba maelekezo na ushauri uliotolewa na Kamati uzingatiwe na utekelezwe haraka zikiwemo kasoro zote zilizobainika ili wananchi wanufaike na utekelezaji huu wa Ilani", amesema Ndugu Siagi.

Kwa upande wa Serikali, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme ambaye hakuwepo baada ya kupata udhuru alisema kuwa, Serikali imepokea kwa unyenyekevu na uzito wa aina yake maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati ya Siasa Mkoa na kwamba ndani ya muda mfupi Serikali itakuwa imetekeleza kikamilivu.

Aidha, Prof. Siza Tumbo ambaye ni Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya RC MNDEME aliongezea kwa kusema kuwa, utekelezaji wa maelekezo ya Kamati utafanyika kwa harhaka sana na kwa weledi mkubwa ili wananchi wanufaike na huduma zitolewazo na Serikali


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa