• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YARIDHISHWA NA ULIPWAJI FIDIA KWA WANANCHI MGODI WA MWADUI

Posted on: November 14th, 2023

Na Shinanga RS

KAMATI ya Maafa ambayo iliundwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kufuatia janga la kubomoka kwa kingo katika Bwawa la Majitope katika Mgodi wa Almasi Mwadui uliopo Wilaya ya Kishapu mkoani  Shinyanga, na kuleta  athari kwa wananchi na kupoteza mali  mbalimbali ikiwemo mashamba na baadhi ya  nyumba, imeridhishwa na namna ambavyo ulipwaji wa fidia kwa wananchi ulivyofanyika.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati hii ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude mara baada ya kufanya ziara  katika Mgodi huo ili kupata taarifa juu ya hatua ya ulipwaji fidia wananchi hao ikiwa ni pamoja na waliokuwa wakidai nyumba zao, sanjali na kukagua ujenzi wa bwawa jipya la Majitope pamoja na kuona Maendeleo ya uzalishaji Almasi katika mgodi huo.

"Kwa ujumla tumeridhishwa na namna ambavyo zoezi la ulipaji wa fidia kwa waathirika wa Majitope katika mgodi huu wa Mwadui ambao ni takribani kaya 304 na kwamba huyu mmoja ambage hajapatikana juhudi ziendelee za kumtafuta ili kumpata na apate stahiki yake," alisema Mhe. Mkude.

Awali akiwasilisha taarifa ya ulipwaji fidia wananchi na maendeleo ya uzalishaji wa Almasi, Mhandisi Mkuu wa Mgodi wa Mwadui Shagembe Mipawa, akimwakilisha Meneja Mkuu wa Mgodi huo, amesema tatizo la kupasuka kingo za Bwawa la Majitope lilitokea Novemba mwaka jana na Wananchi 304 waliathirika na tope hilo.

Amesema mpaka sasa mgodi umefikia asilimia 99.6 kwamba ya ulipaji fidia ambapo kati ya wananchi 304 waliopaswa kukipwa, ni mwananchi 1 tu ndiye ambaye hajalipwa fidia yake na kwamba hajulikani alipo mpaka sasa, huku mgodi ukiendelea kumtafuta sanjali na kuendelea na taratibu zingine za ujenzi wa Makazi Mbadala ya nyumba 47 na kuhamisha Makaburi 14.

Akizungumzia suala uzalishaji wa Almasi, amesema wanaendelea vizuri na tangu waanze uzalishaji Julai mwaka huu hadi kufikia Mwezi Septemba wamezalisha Tani Milioni 1.4 sawa na asilimia 48, Carati Laki 106 sawa na asilimia 64 ya malengo yao.

Pia amewahakikishia wananchi kwamba Bwawa hilo Jipya la Majitope ni salama kabisa, huku wakiendelea pia kulifanyia ukaguzI wa mara kwa mara.

Mwenyekiti wa Kamati ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude (katikati) akielezea jambo wakati kamati ilipotembelea eneo la mgodi


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa