• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KASINYO AWATAKA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI SHINYANGA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU.

Posted on: October 27th, 2025

Na Johnson James, Shinyanga

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Shinyanga, Bakari Kasinyo, ametoa wito kwa wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uzalendo mkubwa ili kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 unafanyika kwa amani, haki na uwazi.

Akizungumza Oktoba 27, 2025 baada ya kutembelea kituo cha mafunzo cha Ukenyenye, Wilayani Kishapu, Kasinyo amesema Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewaamini maafisa hao kusimamia mchakato nyeti wa kidemokrasia, hivyo hawapaswi kufanya makosa au kuruhusu upendeleo wa aina yoyote.

“Mafunzo mnayoyapata ni ya msingi sana. Mnatakiwa kuyatumia kuhakikisha uchaguzi unaendeshwa kwa ufanisi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu. Nawasihi mfanye kazi hii kwa moyo wa kizalendo na kwa kuzingatia maadili ya kazi zenu,” alisema Kasinyo.

Jumla ya wasimamizi na wasimamizi wasaidizi 1,726 wanapatiwa mafunzo ya siku mbili yaliyoanza Oktoba 26 hadi 27, 2025 katika Jimbo la Kishapu, ambapo jumla ya vituo 556 vya kupigia kura vimeandaliwa kwa ajili ya uchaguzi huo.

Kwa upande wao, baadhi ya wasimamizi wakiongozwa na Joel Lwasye, wamesema mafunzo hayo yamewaongezea maarifa na ujasiri wa kusimamia zoezi la upigaji kura kwa ufanisi, huku wakiahidi kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa haki na uwazi ili kupatikana kwa viongozi bora.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa