• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KERO YA BARABARA YA ISOSO YAPATIWA UFUMBUZI – BI MWAMBA

Posted on: November 13th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga Bi. Mwamba Masanja amesema kuwa wameshughulikia kero ya ubovu wa barabara ya Isoso- Mwabusiga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu iliyokuwa inakarabatiwa na kampuni ya Advance Construction Ltd chini ya usimamizi wa TARURA Wilaya ya Kishapu.

Ameyasema haya leo tarehe 13 Novemba, 2024 wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya utendaji kazi wa Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga kwa kipindi cha robo ya kwanza (1) Julai – Septemba kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wake wa kawaida wa ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo.

“Kumekuwa na changamoto za wakandarasi kutekeleza miradi ya barabara chini ya kiwango kinyume na mikataba wanayoingia na Serikali, hivyo TAKUKURU tuliipata taarifa hii na tumefanikiwa kushughulikia kero ya ubovu wa barabara ya Isoso - Mwabusiga iliyopo Kishapu ambayo Kampuni ya Advance Construction Ltd ilikuwa ikikarabati”, amesema Bi Mwamba

Aidha ameongeza kuwa watuhumiwa hao ambao wamehusika na  ukarabati wa barabara ya Isoso – Mwabusiga ambao ni Mhandisi Juma Mkela msmamizi mkuu wa kampuni ya Advance Construction, Mhandisi wa mafunzo TANROAD Shinyanga Charles Emmaneul pamoja na Mhandisi Wilfred Gutta Meneja wa TARURA Kishapu, tayari wamefikishwa mahakamani na kuamriwa kurejesha kiasi chote cha fedha Shilingi Milioni 29.

Aidha Bi Mwamba amewaomba wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kupiga simu bure namba 113 ili kuripoti vitendo vinavyoashiria ubadhilifu wa fedha za miradi ya maendeleo ambayo inaendelea kutekelezwa katika Mkoa wa Shinyanga.

TAKUKURU inaendelea kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kutoa ushirikiano kwa Serikali ili kuhakikisha miradi yote inayoendelea katika Mkoa wetu inakamilika kwa ubora kama ilivyopangwa.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA TATU YA MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA SABASABA – 2025

    July 01, 2025
  • RC. ANAMRINGI MACHA AKABIDHI OFISI KWA RC. MBONI MHITA

    July 01, 2025
  • RC. MBONI MHITA ASHIRIKI KIKAO KILICHOONGIZWA NA MHE. MCHENGERWA JIJINI DODOMA

    June 28, 2025
  • NAIPONGEZA OFISI YA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA KWA URATIBU MZURI WA USHIRIKI WA WAFANYABIASHARA KATIKA MAONESHO YA SABASABA - MASUDI KIBETU

    June 28, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa