• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KIJIJI CHA SAYU NDIYO KINARA WA KILIMO CHA PAMBA MKOA WA SHINYANGA – RC MACHA

Posted on: February 19th, 2025

Na Paul Kasembo, SHY DC,

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa, Kijiji cha Sayu kilichopo Kata ya Pandagichiza Wilaya ya Shinyanga ndiyo kinara wa uzalishaji wa zao la pamba Mkoa wa Shinyanga kwani kina wakulima ambao wamelima pamba na kupata kwa wingi zaidi tofauti na maeneo mengine.

RC Macha ameyasema hayo leo Februari 19, 2025 wakati akihitimisha ziara ya kukagua na kuhamasisha kilimo cha pamba mkoani Shinyanga ambapo alitembelea Halmashauri ya Wklaya ya Ushetu, Kishapu na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambapo huku akisisitiza kuwa katika maeneo yote aliyotembelea lakini Kijiji cha Sayu ndiyo kimeibuka kinara katika uzalishajin wa pamba kulinganisha na maeneo mengine.

“Niwapongeze sana ninyi wakulima wa pamba katika Kijiji hiki ya Sayu na kuwa kinara wa uzalishaji wa zao la pamba hapa Shinyanga, nimepita na kutembelea wakulima wengi lakini ninyi mmekuwa mfano bora wa kuzalisha kilo nyingi kwa hekari moja ambapo hapa kuna mwenye kilo 2200 kwa hekari, kilo 1800, kilo 1600 na wa chini kabisa alipata kilo 1340 kwa hekari 1, huu ni mfano bora sana na wakuigwa” amesema RC Macha.

RC Macha ameongeza kuwa Serikali ina malengo ya kuhakikisha wakulima wanafurahia kilimo cha pamba na kuvuna kuanzia kilo 1200 na kuendelea kwa hekari moja katika maeneo yote mkoani Shinyanga ingawa Wilaya ya Shinyanga inaonesha wakulima wengi wamekuwa wakinufaika na kupata faida kubwa tofauti na maeneo mengine kwani kwa hekari moja wanapata zaidi ya kilo 1000.

Aidha RC Macha amempongeza na kumtolea mfano ndugu Andrea Maganga mkulima wa pamba kutoka Kijiji cha Sayu, Kata ya Pandagichiza aliyeibuka mshindi wa pili wa kilimo cha pamba nchini na kupewa zawadi ya Tzs. Milioni 5 ambaye hulima kwa kuzingatia kipimo cha Sentimita 60x30 kwani kina tija zaidi na mkulima anaweza akapata kilo takribani 2200 kwa hekari 1.

Awali akizungumza na wakulima, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Wakili) alimtaka Afisa Ugani Kilimo kupima ukubwa wa mashamba ya pamba ili ifahamike kitaalam ukubwa wake na uwekwe kwenye kumbukumbu sahihi za ofisi na kwa matumizi ya rejea pia.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa