• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

Posted on: May 26th, 2025

Shinyanga, Mei 26, 2025 – Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Julius Mtatiro (Wakili), kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, amewataka wastaafu kuzingatia utulivu na ustawi wa maisha baada ya kustaafu, akisisitiza kuwa kipindi hicho ni muda wa kupumzika baada ya utumishi wa muda mrefu kwa Umma.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (Retirees’ Association of Tanzania - REAT) Mkoa wa Shinyanga, iliyofanyika katika Ukumbi wa CCM Mkoa, Mhe. Mtatiro amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kushughulikia changamoto za wastaafu na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo ya Taifa.

Mhe. Mtatiro amewahimiza wastaafu kujiunga katika vikundi vya kiuchumi ili kuanzisha miradi endelevu, huku akibainisha kuwa Serikali ipo tayari kutoa mikopo isiyo na riba kwa makundi hayo ili kuwawezesha kuendeleza maisha yao kwa heshima na utu.

Aidha, ametoa rai kwa wazee kushiriki katika kulinda maadili ya jamii kwa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kama vile ubakaji na ulawiti, na kuwahimiza kutoa malezi bora kwa watoto kwa kuzingatia tahadhari mbalimbali ndani ya familia. Pia amesisitiza umuhimu wa kuandika wosia, akieleza kuwa ni hatua muhimu ya maandalizi ya maisha baada ya wao kuondoka.

Vilevile, Mhe. Mtatiro amewaasa wazee kuwa mabalozi wa amani na kuhimiza ushiriki wa vijana katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Kwa upande wake, Rais wa Umoja wa Wastaafu Tanzania (REAT), Alhaj Dauda Bilikesi, amesema lengo kuu la umoja huo ni kuimarisha mshikamano, kutambua mchango wa wastaafu kwa Taifa na kuendeleza utetezi wa haki na maslahi yao baada ya utumishi.

Akiwasilisha risala ya REAT, Mwalimu Mstaafu Magdalena Faustine alisema umoja huo unalenga kuwaunganisha wastaafu, kushirikiana na Serikali katika kutetea haki zao, na kuwawezesha kushiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi, sambamba na kutoa elimu kuhusu haki zao.

Mratibu Mkuu wa REAT, Mwalimu Ezekiah Oluoch, alieleza kuwa Umoja huo ulianzishwa mwaka 2021, na unawahusisha wastaafu kutoka sekta ya umma na binafsi wanaopokea mafao kupitia mifuko ya hifadhi ya jamii ya PSSSF, NSSF na Hazina.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa