• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA SHINYANGA ( SHUWASA) YATOA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAKE KWA MWAKA 2022/2023

Posted on: June 30th, 2023


Mamlaka ya Majisafina Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) imetoa taarifa yake ya utekelezaji wa majukumu yake katika kuwahudumia wananchi wake kwa mwaka wa fedha 2022/2023 huku ikiahidi maboresho makubwa zaidi Tinde, Didia, Shinyanga Manispaa na Iselamagazi.

Akitoa taarifa mbele ya waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka CPA. Sarah Emmanuel amesema kuwa kwa sasa SHUWASA inatoa huduma kwa wakazi 282,698 lakini waliofikiwa na huduma ya majisafi moja kwa moja kupitia maunganisho ya majumbani na magati kww maeneo yote yanayohudumiwa na Mamlaka ni wakazi 186,580.

 

"Ndugu waandishi wa habari kwa ujumla mahitaji ya maji kwa wakazi wa Manispaa ya Shinyanga na miji midogo ya Tinde, Didia na Iselamagazi ni mita za ujazo 18,833 kwa siku, ambapo kwa mwezi Mei 2023 Mamlaka ilisambaza maji yenye mita za ujazo 417, 977 sawa na wastani wa mita za ujazo 13,483,1 kwa siku na kati ya maji hayo 18.6% yalipotea kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo kupasuka mabomba na njia nyingine zisizo rasmi," alisema CPA. Sarah.

SHUWASA inatekeleza miradi minne (4) midogo ndani ya eneo la Manispaa ya Shinyanga yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 1.6 fedha toka Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji ambapo kwa eneo la Tinde Mamlaka inasambaza mtandao wa maji Kilomita 8.1 kwa awamu ya kwanza ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ujenzi wa mradi wa Tinde-Shelui.

Eneo jingine ni Didia ambako Mamlaka inasambaza mtandao wa maji Kilomita 8.1 (KM 1.9 bomba kuu na KM 6.2 bomba za usambazaji) ambao upo 62% na unatarajiwa kukamilika Julai, 2023 ambapo Didia pia panajengwa Tangi la maji lenye ujazo wa mita za ujazo 100 ni mradi ambao upo katika hatua za majaribio.

Iselamagazi ni moja ya eneo linalohudumiwa na Mamlaka ambapo zaidi ya Milioni 106 zimetengwa kwa ujenzi wa mtandao wa bomba za usambazaji KM 3.14 fedha kutoka Mfuko wa Maji ikiwa zaidi ya Milioni 31 zimepokelewa na Mamlaka na kuanza ujenzi wa KM 1.75 unaotarajiwa kukamilika Julai 2023 na kumufaisha wakazi zaidi ya 3000.

SHUWASA na SHIRIKA LA MAENDELEO LA UFARANSA (AFD) inatekeleza mradi mkubwa wenye thamani ya EURO 76 uliosainiwa Juni 20, 2022 ambapo SHUWASA kupitia Wizara ya Fedha imepokea EURO 10 na Zabuni mbili za Wahandisi Washauri pamoja na Usaidizi wa Mamlaka zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Aidha SHUWASA haijaanza kutoa huduma ya MAJITAKA wal uondoaji wa majitaka, hata hivyo inachakata TOPE KINYESI kwa kushirikiana na Manispaa ya Shinyanga kupitia mtambo uliopo Kata ya Kizumbi uliojengwa kwa ufadhiri wa SNV.

Pamoja na ufanisi huu mzuri lakini SHUWASA pia inakabiliwa na changamoyo kadhaa ikiwamo uchakavu wa miundombinu, wadaiwa wakubwa kutolipa madeni lakini imejipanga kuboresha huduma kwa wateja wake wa Manispaa ya Shinyanga, Mji mdogo wa Tinde, Didia na Iselamagazi, kuendelea kutoa elimu kwa umma nk.

Kwa ujumla Mamlaka inayo vyanzo vyake vikuu vya maji vitatu (3) ambavyo ni 1. Visima virefu (Bushora na Tinde 2. Bwawa la Ning'hwa na 3. Maji ya Ziwa Victoria.





Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa