• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MFUMO WA STAKABADHI GHALANI WAONGEZA FURSA ZAIDI KWA WAKULIMA - MHE. DKT. JAFO

Posted on: March 13th, 2025

Na. Paul Kasembo.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Seleman Jafo amesema kuwa ujio wa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani umewawezeaha na kuwaongezea fursa zaidi wakulima nchini wakiwemo wa Mkoa wa Shinyanga.

Mhe. Dkt. Jafo ameyasema hayo leo Machi 13, 2025 wakati akitoa maelezo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo iliyotembelea na kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Serikali juu ya matumizi sahihi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ambapo Kamati imeshuhudia hayo katika Ghala la Mboje lililopo Manispaa ya Shinyanga na kusisitiza kuwa mfumo unaongeza ushindani zaidi miongoni mwa wanunuzi.

"Mhe. Mwenyekiti na wajumbe wa Kamati, nipende kusema kuwa ujio na matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani umekuja na ongezeko la fursa nyingi zaidi kwa wakulima wetu kwa kuwa hivi sasa wanunuzi ambao ndiyo wafanyabiashara wananunua kwa ushindani sana kulingana na msimamo wa bei ya soko na wingi wao. Na hilo ndiyo lilikuwa lengo kuu la Serikali kuhakikisha mkulima anaanza kunufaika na kilimo cha mazao mbalimbali yakiwemo ya Choroko na Dengu hapa Shinyanga," alisema Dkt. Jafo.

Akitoa ufafanuzi, umuhimu na faida ya matumizi ya mfumo, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi Ghalani ndg. Asangye Bangu alisema kuwa katika mikoa ya Kagera, Mwanza na Shinyanga mfumo haukuweza kutumika kutokana na kutokuwa tayari kwa wadau mbalimbali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha alimueleza Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati kuwa, awali haikuwa kazi rahisi sana kufikia maridhiano kati ya Serikali ya Mkoa na Wafanyabiashara na kuanza kwa matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi ya Ghala mkoani Shinyanga. Lakini baada ya majadiliano na utoaji wa elimu kwa kushirikiana na wataalam wa WRRB waliweza kufanikiwa na sasa Serikali imeanza kuona mapinduzi makubwa ya wakulima na wafanyabiashara ambapo pande zote zinanufaika.

Akihitimisha ukaguzi wa Ghala na kuona faida ya matumizi ya mfumo, Mhe. Deodatus Mwanyika (MB) ambaye ni Mwenyekiti kwa niaba ya Kamati amekiri kuridhishwa na utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ya ghala hususani mkoani Shinyanga.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa