• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. MNDEME AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE MKOANI SHINYANGA KUANZISHA DAWATI NA OFISI MAALUMU KWA AJILI YA KURATIBU NA KUSHUGHULIKIA MASUALA YA MACHINGA

Posted on: July 22nd, 2023

Na. Shinyanga RS

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme amiziagiza Halmashauri zote Mkoani Shinyanga kuanzisha Dawati na Ofisi Maalumu itakayokuwa na jukumu kuratibu na kushughulikia mambo yote yanayohusu Machinga katika maeneo yao.

Agizo hilo amelitoa leo Julai 22, 2023 wakati akifungua rasmi Kongamano la Shirikisho la Umoja wa Machinga Mkoa wa Shinyanga lililofanyika Wilaya ya Kahama lenye lengo la kumpongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoifanya kwa watanzania wote na hasa Machinga nchi nzima.

Mhe. Mndeme ametoa agizo hilo baada ya kupokea risala ya Shirikisho la Machinga lilisomwa kwake na Mwenyekiti wa SHIUMA TAIFA ndugu Ernest Matondo ambayo ndani yake ilieleza umuhimu wa uwepo wa Dawati na Ofisi Maalumu katika kila Halmashauri ambapo Manispaa ya Kahama wao walikwisha anza kutekeleza mpango huu.

"Nimeskiliza kwa makini lisala yenu, yapo tutakayo yabeba kwenda kuyatekeleza, yapo mengine nayatolea majibu hapa hapa na sasa naagiza kila Halmashauri hapa Mkoani Shinyanga ianzishe haraka Dawati na Ofisi Maalumu itakayokuwa na jukumu la kuratibu na kushughulia mambo ya Machinga peke yake agizo hili lianze kutekelezwa haraka iwezekanavyo," alisema Mhe. Mndeme.

Kando na hayo, pia SHIUMA kwa kauli moja wamesema wanamuunga mkono Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maamuzi ya Serikali ya Tanzania kuingia mkataba wa uboresha wa utoaji huduma katika Bandari yetu na Serikali ya Dubai na kwamba SHIUMA ipo nae baga kwa bega huku wakimtaka kutowasikiliza hao wasiokuwa na nia njema na Serikali.

Aidha Kongamano hili pia limelenga kupinga mambo yote ya ukatili wa kijinsia na mmomonyoko wa maadili katika jamii zetu, kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kupendezesha maeneo yetu kwa faida ya urithi wa Nchi na vizazi vijavyo.

SHIUMA wameipongeza sana Serikali ya Mkoa wa Shinyanga kwa kuwezesha kupatikana kwa suluhu ya machinga ambapo imejenga Soko la Ngokolo (mtumbani), Soko la Ibinzamata, Soko la C. D. T stendi ya Kahama, Soko lq Machinga (mnara wa voda) na soko la mbogamboga Mhunze lililopo Kishapu.

Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) Tanzania ulipata usajili wake wa awali mwaka 2014 kwa jina la Umoja wa Machinga Tanzania.

Mwaka 2018 Umoja ulianza kuimarika zaidi baada ya kufanya kikao kilichojumuisha Mikoa 14 kwa kushirikiana na OR - TAMISEMI  chini ya Waziri Mhe. Jafo S. Jafo, Wizara ya Fedha kupitia Naibu Waziri Mhe. Ashantu Kijaji mkutano ambao ulifanyika Dodoma.

Ilipofika Feb 19, 2019 SHIUMA ilifanya kikao ambacho kilijumuisha  Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na Mei 16, 2022

Picha ikionesha baadhi ya machinga wakiwa kwenye kongamano Kahama-Shinyanga

Mhe. Mndeme akipokea Cheti cha Pongezi kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri ya kuwawezesha machinga katika kutekeleza kazi zao nchi nzima

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa