• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. MTATIRO AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU

Posted on: June 27th, 2024

Na. Paul Kasembo, USHETU DC.

MUWAKILISHI wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Julius Mtatiro (Adv) ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kwa kuonesha uwezo mkubwa wa kuandaa, kujibu, na kuwasilisha hoja zinazohusu Utekelezaji wa Mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo ilikuwa na jumla ya hoja 32 na 16 kati ha hizi zilikaguliwa na kufungwa, 15 zipo kwenye hatua ya utekelezaji huku 1 haijatekelezwa huku akimtaja Bi. Hadija Kabojela kama Mkurugenzi na mwanamama wa kuigwa kama mfano.

Mhe. Mtatiro ameyasema leo tarehe 27 Juni, 2024 katika Baraza Maalum la CAG ambapo pamoja na mambo mengine Mhe. Mtatiro amewapongeza sana Waheshimiwa Madiwani wote na kipekee kwa Waheshimiwa wanamama ambao wameonesha uwezo mkubwa sana wa kuchambua, kujenga na kupambania hoja kwa lengo la kuiletea maendeleo Ushetu, kutetea haki na mali za Wanaushetu tena kwa kutumia na kusoma Kabrasha kwa kujiamini, utulivu na uzalendo mkubwa zaidi.

"Kwa dhati kabisa naipongeza sana Ushetu DC kwa namna ambavyo mmeonesha uwezo mkubwa wa kuandaa, kujibu na kuwasilisha taarifa zenu zinazohusu mapendekezo ya CAG, pia waheshimiwa madiwani wote hasa wanamama, mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Gagi Lala, Mkurugenzi wa Ushetu Bi. Hadija Kabojela na watalaam hakika mnastahili pongezi hizi mmekuwa mfano wa kuigwa kulinganisha na Halmashauri nyingine ambazo nimepita na kuona utekelezaji wa hili," amesema Mhe. Mtatiro.

Ushetu inatajwa kuwa na hoja chache zaidi kulinganisha na Halmashauri nyingine hapai Shinyanga ambapo hoja za nyuma zilikuwa 78, zimejibiwa 70 na kubakia 8 ambazo zipo kwenye hatua ya utekelezaji jambo ambalo limepongezwa sana pia na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo ambaye amesema kuwa kipekee ameshuhudia mshikamamo mkubwa wa madiwani, Mhe. Mbunge na wataalam wakiongozwa na Mkurugenzi Bi. Hadija Kabojela.

Akiahirisha mkutano huu, Mhe. Gagi amesema kuwa anapokea pongezi hizi zote, maelekezo na ushauri uliotolewa wote na kwamba wanakwenda kuanza kutekeleza huku akisisitiza kuwa kwa kauli moja, baraza la madiwani linaazimia na kuelekeza kuwa wale wote wanaodaiwa kutokana na mkopo wa fedha za asilimia 10 za wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambao hawajalipa watafutwe na walipe fedha hizo ili Halmashauri iweze kuondokana na hoja za CAG na pia kwa kufanya hivyo kutawezesha na wengine kukopa na hivyo kuinua uchumi wa wananchi wa Ushetu.


HABARI PICHA

Pichani ni Mhe. Julius Mtatiro (Wakili)

Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo

Mhe. Gali Lala Gagi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ushetu

Picha ikionesha sehemu ya waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Ushetu

Bi. Hadija Kabojela, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa