• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AWATUA NDOO KICHWANI AKINAMAMA WILAYANI KISHAPU - MHE. KUNDO

Posted on: July 28th, 2024

Na. Paul Kasembo, Kishapu.

NAIBU Waziri wa Maji Mhe. Eng. Mathew Kundo amesema uwepo wa miradi ya maji mingi na mikubwa yenye tija kwa wananchi ambayo inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoani Shinyanga inakusudia kutekeleza nankutafsiri kwa vitendo maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya mtua ndoo mama kichwani.

Mhe. Kundo ameyasema haya wakati akikagua utekelezaji wa mradi wa RUWASA wilayani Kishapu ambapo pamejengwa Tangi la maji lenye ujazo wa Lita laki mbili litakaloweza kuhudumia maji safi na salama kwa vijiji 5 zaidi ya wakazi elfu kumi na tano katika Kata ya Uchungai wilayani Kishapu huku akitia wito kwa wananchi kuitunza miundombinu hii muhimu pamoja na vyanzo vya maji.

"Ndugu zangu Wanangundangali hapa Kishapu niwaeleze ukweli kabisa, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewatua ndoo akina mama hapa katika Kata ya Uchunga Kishapu, ambapo kupitia mradi huu wa RUWASA mnaanza kunufaika na maji safi na salama wa vijiji vitano, haya ndiyo maono ya Mhe. Rais wetu kwa wananchi wake na jambo kubwa ni kuhakikisha mnatunza miundombinu hii na vyanzo vyake vya maji," amesema Mhe. Kundo.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kundo amempongeza sana Mhandisi Julieth Payovera wa RUWASA Mkoa wa Shinyanga kwa namna ambavyo anatekeleza kazi zake kwa weledi na ufanisi mkubwa zaidi kwa kushirikiana na wasaidizi wake pamoja na mamlaka nyingine huku akisema utendaji kazi huu ni kilelezo cha uwepo wa watumishi wazalendo na wachapakazi.

Kwa kifupi, ujenzi  wa  mradi  wa  Maji ya  Bomba Seseko Ngundangalii unatekelezwa  na  Mkandarasi  M/s Otonde Construction and General Supplier  wa Mwanza kwa  Mkataba  No. AE-102/2022/2023/SHY/W/15 chini  ya Usimamizi  wa  RUWASA  Wilaya ya Kishapu  wakishirikiana  na  RUWASA  mkoa wa  Shiyanga.  Muda wa  utekelezaji ni  siku 365  sawa  na  mwaka  mmoja, mradi  ulianza  kujengwa  mnamo tarehe 5/3/2023 na ujenzi wake umekamilika mwezi Juni, 2024.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa