• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MHE. UMMY ASISITIZA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WANANCHI.

Posted on: July 14th, 2023
Na.Shinyanga RS.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewasisitiza watalaamu wa afya kuboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wananchi huku akiangazia zaidi katika matumizi ya lugha na kauli zenye staha kwa wananchi sambamba na uhakika wa upatikanaji wa dawa, uhakika wa upatikanaji wa vipimo vya maabara kwa wananchi kwa lugha vipimo kwa kuzingatia taaluma, maadili, viapo, weledi, kanuni na sheria za kitabibu lengo ni kuokoa maisha ya wagonjwa pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa watoto wachanga hasa wenye uzito mdogo zaidi waweze kuokolewa huku akisema kwa ujumla Sekta ya afya Kishapu ipo salama kabisa.

Mhe. Ummy alisema watumishi wa afya ataendelea kuwakumbusha wajibu na majukumu yao lakini akawataka kutofanya makosa katika taaluma zao jambo ambalo laweza kumpelekea kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za mabalaza ambapo yaweza kumfutia kibali au leseni yake jambo ambalo asingependa litokee.

Ndugu zangu wataalamu wa afya, nipende kuwasisitiza sana katika kuzingatia weledi, maadili, miiko na utu katika utoaji wa huduma kwa wananchi wetu huku tukitumia muda mwingi zaidi kutatua kero na kupunguza malalamiko kwa wananchi wetu na kwa kuhakikisha pia madaktari mnaandika dawa kwa kufuata miongozo ya vitabu vya dawa vya taifa ili kuondoa malalamiko kwa wagonjwa wetu," alisema Mhe. Ummy.

Akitoa salamu za Wilaya Mbunge wa kishapu Mhe. Boniphace Butondo alisema kuwa Kishapu kuna upungufu wa watumishi zaidi ya 70% jambo ambalo linazorotesha utoaji wa huduma ukizingatia kuwa kishapu ina jumla ya Kata 29 ambapo Kata zina Vijiji 9 na unakuta kuna watumishi wanne tu na nyumba za watumishi ni chache sana kulingana na mahitaji halisi huku akielezea pia suala la maboma zaidi ya 50 ambayo hayajakamilika.

"Mhe. Waziri, kuna suala zima la Zahanati za Kishapu kutokamilika kwa wakati ni kwakuwa Mhe. Mbunge, Madiwani, Mkurugenzi sote tunahamasisha wananchi kuanzisha majengo ya afya ambapo tukiamini kuwa yakifkia hatua flani Serikali itasapoti kukamilisha, sasa kuna maboma zaidi ya 50 hayajakamilishwa , lakini iwapo yangekamilika majengo hayo ni yangesogeza huduma karibu na wananchi wetu," alisema Mhe. Butondo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude alisema Hospitali ya Wilaya inakwenda vizuri sana, ambapo kwa sasa wamepokea fedha zaidi ya biloni 2 zilizowezesha kujenga majengo mengi jambo ambalo linapelekea kuongeza na kuboresha huduma zaidi sanjari usimamizi mzuri kwa watumishi.

"Tunaendelea kupokea fedha nyingi za dawa, tunasimamia na kudhibiti utoaji wa dawa kwa wananchi, tumeongeza vifaa tiba, majengo na huduma tumeboresha zaidi jambo ambalo linapelekea kuondoa malalamiko kwa wananchi wetu wa Wilaya ya Kishapu," alisema Mhe. Mkude.

Pia Mhe. Mkude alisema kuwa suala la maadili na nidhamu kwa watumishi wa Sekta ya afya kishapu limedhibitiwa na sasa hakuna tena tabia hizo mbaya ambazo awali zilikuwa zikiripotiwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa na kwamba hakuna malalamiko.

Hoja nyingine ilitolewa ni ya upungufu wa gari la wagonjwa (Ambulance) likitajwa kuwa ni muhimu kuongezwa kulingana na ukubwa wa Wilaya ambapo kuna vituo vya afya 8 na vitatu vinakamilishwa hivyo vitakuwa 11 pia kwa kuzingatia jiografia ya Wilaya ilivyo hivyo wakaomba kuongezwa kwa ambulance angalau zifikie ( 3 ) zaidi badala ya moja kama ambavyo tumepangiwa na Serikali hoja ambayo ilijibiwa palepale kwa kupokelewa na Mhe. Waziri alikubaliana na ombi hilo huku akisema zitaletwa ambulance tatu kama walivyoomba.











































MHE. UMMY ASISITIZA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WANANCHI.


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewasisitiza watalaamu wa afya kuboresha zaidi utoaji wa huduma kwa wananchi huku akiangazia zaidi katika matumizi ya lugha na kauli zenye staha kwa wananchi sambamba na uhakika wa upatikanaji wa dawa, uhakika wa upatikanaji wa vipimo vya maabara kwa wananchi kwa lugha vipimo kwa kuzingatia taaluma, maadili, viapo, weledi, kanuni na sheria za kitabibu lengo ni kuokoa maisha ya wagonjwa pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma kwa watoto wachanga hasa wenye uzito mdogo zaidi waweze kuokolewa huku akisema kwa ujumla Sekta ya afya Kishapu ipo salama kabisa.


Mhe. Ummy alisema watumishi wa afya ataendelea kuwakumbusha wajibu na majukumu yao lakini akawataka kutofanya makosa katika taaluma zao jambo ambalo laweza kumpelekea kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za mabalaza ambapo yaweza kumfutia kibali au leseni yake jambo ambalo asingependa litokee.


Ndugu zangu wataalamu wa afya, nipende kuwasisitiza sana katika kuzingatia weledi, maadili, miiko na utu katika utoaji wa huduma kwa wananchi wetu huku tukitumia muda mwingi zaidi kutatua kero na kupunguza malalamiko kwa wananchi wetu na kwa kuhakikisha pia madaktari mnaandika dawa kwa kufuata miongozo ya vitabu vya dawa vya taifa ili kuondoa malalamiko kwa wagonjwa wetu," alisema Mhe. Ummy


Akitoa salamu za Wilaya Mbunge wa kishapu Mhe. Boniphace Butondo alisema kuwa Kishapu kuna upungufu wa watumishi zaidi ya 70% jambo ambalo linazorotesha utoaji wa huduma ukizingatia kuwa kishapu ina jumla ya Kata 29 ambapo Kata zina Vijiji 9 na unakuta kuna watumishi wanne tu na nyumba za watumishi ni chache sana kulingana na mahitaji halisi huku akielezea pia suala la maboma zaidi ya 50 ambayo hayajakamilika.


"Mhe. Waziri, kuna suala zima la Zahanati za Kishapu kutokamilika kwa wakati ni kwakuwa Mhe. Mbunge, Madiwani, Mkurugenzi sote tunahamasisha wananchi kuanzisha majengo ya afya ambapo tukiamini kuwa yakifkia hatua flani Serikali itasapoti kukamilisha, sasa kuna maboma zaidi ya 50 hayajakamilishwa , lakini iwapo yangekamilika majengo hayo ni yangesogeza huduma karibu na wananchi wetu," alisema Mhe. Butondo.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude alisema Hospitali ya Wilaya inakwenda vizuri sana, ambapo kwa sasa wamepokea fedha zaidi ya biloni 2 zilizowezesha kujenga majengo mengi jambo ambalo linapelekea kuongeza na kuboresha huduma zaidi sanjari usimamizi mzuri kwa watumishi.


"Tunaendelea kupokea fedha nyingi za dawa, tunasimamia na kudhibiti utoaji wa dawa kwa wananchi, tumeongeza vifaa tiba, majengo na huduma tumeboresha zaidi jambo ambalo linapelekea kuondoa malalamiko kwa wananchi wetu wa Wilaya ya Kishapu," alisema Mhe. Mkude.


Pia Mhe. Mkude alisema kuwa suala la maadili na nidhamu kwa watumishi wa Sekta ya afya kishapu limedhibitiwa na sasa hakuna tena tabia hizo mbaya ambazo awali zilikuwa zikiripotiwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa na kwamba hakuna malalamiko.


Hoja nyingine ilitolewa ni ya upungufu wa gari la wagonjwa (Ambulance) likitajwa kuwa ni muhimu kuongezwa kulingana na ukubwa wa Wilaya ambapo kuna vituo vya afya 8 na vitatu vinakamilishwa hivyo vitakuwa 11 pia kwa kuzingatia jiografia ya Wilaya ilivyo hivyo wakaomba kuongezwa kwa ambulance angalau zifikie ( 3 ) zaidi badala ya moja kama ambavyo tumepangiwa na Serikali hoja ambayo ilijibiwa palepale kwa kupokelewa na Mhe. Waziri alikubaliana na ombi hilo huku akisema zitaletwa ambulance tatu kama walivyoomba.






















ReplyForward











































Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa