• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Mkandarasi Barabara za Manispaa ya Shinyanga aagizwa kukamilisha kwa wakati

Posted on: May 14th, 2018

Mkandarasi anayetengeneza barabara kwa kiwango cha lami katika Manispaa ya Shinyanga chini ya mpango wa uimarishaji Miji (ULGSP) Jassie & Co. Ltd (JASCO), ametakiwa kukamilisha kazi iliyobaki kiasi cha kilomita 8.9 kwa wakati uliopangwa vinginevyo atachukuliwa hatua.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo amemuagiza Mkandarasi huyo mapema leo alipotembelea Mkoani Shinyanga kwa lengo la kukagua ujenzi wa barabara hizo ulioanza tangu mwaka 2016.

Mhe. Jafo amesema atarudi baada ya miezi mitatu baada ya Mkandarasi kumuhakikishia kuwa, baada ya muda huo atakuwa amekamilisha kazi hizo ikiwemo uwekaji wa taa za barabarani baada ya changamoto zilizokuwepo kufanyiwa kazi.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemueleza Waziri Jafo kuwa, endapo Mkandarasi huyo atakwenda kinyume atachukuliwa hatua za kisheria kwani amekuwa na kazi maeneo mengi hali inayochangia kufanya kazi isiyoridhisha.

Mradi huo wa ujenzi wa barabara za lami chini ya ULGSP ulianza mwaka 2016 ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga iliingia mkataba na JASCO kujenga jumla ya kilomita 13.1 kwa gharama ya zaidi ya sh. Bil. 15, lakini hadi mwishoni mwa mwaka jana 2017 ni km 4 tu ndiyo zilikuwa zimewekwa lami wakati km 4.43 zimejengwa tuta kwa ajili ya maandalizi ya kuwekwa lami.

Aidha, ujenzi huo ulisimama kwa takribani miezi 9 tangu Septemba mwaka 2017 kutokana na Mkandarasi kudai kutatuliwa baadhi ya changamoto ikiwemo marekebisho ya mkataba ambapo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa, ziliweka sawa maeneo yaliyohitaji kutekelezwa na ujenzi umeanza tena mwezi Mei,2018 ukitarajiwa kukamilika tarehe 23 Oktoba, 2018.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Bw. Gofrey Mwangulumbi amemueleza Mhe. Jafo kuwa, changamoto ya fedha ilitokana na kuja kwa fedha ambazo hazikuwa na mchanganuo hivyo kuchelewesha ufungaji wa mkataba. 

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa