• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MKANDARASI CHICO, FUNGA TAA UWANJANI HARAKA ILI UTUMIKE MASAA 24 - MHE. MAJALIWA.

Posted on: February 16th, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

WAZIRI Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Mkandarasi anayefanya Ukarabati mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga aitwae China Hennan International Corperation Group Co. Ltd (CHICO) kuagiza taa na kuzifunga haraka ili uwanja utakapoanza kutumika uweze kufanya kazi masaa 24 na ukizingatia CHICO hadai pesa yoyote katika Kandarasi hii inayotajwa kuwa bora na yenye tija zaidi kwa Mkoa wa Shinyanga, Simiyu, Geita na maeneo jirani kwa ujumla.

Mhe. Majaliwa ameyasema hayo leo februari 16, 2025 baada ya kukagua ujenzi wa jengo la abiria lililopo uwanja wa ndege wa Shinyanga na ambalo ujenzi wake umetajwa kufikia asilimia 50 kukamilika huku akimsisitiza CHICO kuongeza kasi ya ujenzi na kufanya afanye kazi usiku na mchana lengo likiwa ni kukamilisha mradi huu kabla ya mwezi wa 8 uliotajwa katika mkataba.

"Wito wangu kwako Mkandarasi CHICO, agiza taa na uzifunge hapa uwanjani haraka kwani uwanja huu utakuwa ukifanya kazi masaa 24 na ukizingatia una viwango vyote vya Kimataifa na ndiyo maana Serikali iliongeza fedha za kuongeza urefu wa njia ya kuruka na kutua kutoka KM 2 hadi 2.2," amesema Mhe. Majaliwa.

Akimkaribisha kukagua jengo hilo, Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Joel Mwambungu alimueleza Mhe. Majaliwa kuwa, katika kuhakikisha ukarabati mkubwa unafanyika, zaidi ya Milioni 700 zililipwa kwa wananchi wa maeneo hayo ili kupisha utekelezwaji wa mradi huo mkubwa na wa kimkakati zaidi kwa Mkoa wa Shinyanga na maeneo jirani.

Mha. Joel alisisitiza kuwa, uwepo wa mradi huu mkubwa umewezesha wananchi takribani 160 kupata ajira za muda huku 130 kati ya hao ni wazawa wa Shinyanga.

"Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, katika kuhakikisa mradi huu mkubwa na wa kimkakati unatekelezeka bila malalamiko, Serikali iliwalipa Tzs. Milioni zaidi ya 700 wananchi wa maeneo haya ya Ibadakuli hapa Manispaa ya Shinyanga ili kupisha mradi huu kutekelezwa, na pia zaidi ya wananchi 160 walipata ajira ya muda huku 130 kati ya hao ni wazawa wa Mkoa huu wa Shinyanga," amesema Mha. Joel.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa