• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MKURUGENZI MKUU WA TANESCO AMKABIDHI MKUU WA MKOA WA SHINYANGA JIKO LA KISASA LA UMEME

Posted on: June 9th, 2025

#shinyanga_rs

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Lazaro Twange, amefanya ziara rasmi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Anamringi Macha pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya TANESCO na uongozi wa Mkoa.

Katika mazungumzo yao, viongozi hao walisisitiza umuhimu wa upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hususan kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga. Mha. Twange alieleza kuwa TANESCO inaendelea kuboresha huduma zake na kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi bora ya umeme, hasa kwa kutumia vifaa vinavyotumia nishati kidogo.

Akiwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mha. Twange alikabidhi rasmi jiko la kisasa linalotumia umeme kwa kiwango kidogo kwa Mhe. Anamringi Macha, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya shirika hilo katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi, rafiki kwa mazingira na nafuu kwa matumizi ya kawaida ya nyumbani.

"Jiko hili ni suluhisho linalolenga kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, hivyo kuchangia katika uhifadhi wa mazingira na afya ya wananchi," alisema Mhandisi Twange.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Anamringi Macha, alimshukuru Mkurugenzi huyo kwa ujio wake na zawadi ya jiko hilo. Aliahidi kuendelea kushirikiana na TANESCO katika kampeni za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ili kufikia malengo ya kitaifa ya uhifadhi wa mazingira na kuboresha maisha ya wananchi.



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI MKUU WA TANESCO AMKABIDHI MKUU WA MKOA WA SHINYANGA JIKO LA KISASA LA UMEME

    June 09, 2025
  • MRADI WA TABLET KWA SHULE ZA MSINGI WATAMBULISHWA NGAZI YA MKOA WA SHINYANGA NA WILAYA

    June 03, 2025
  • SHINYANGA KUNUFAIKA NA MIRADI YA REA, WAUZIWA KWA RUZUKU MITUNGI 13000

    June 02, 2025
  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa