• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AMPONGEZA MRAJIS BI, HILDA BONIPHACE KWA UTENDAJI KAZI MZURI

Posted on: July 2nd, 2023

Na. Paul Kasembo - Tabora

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Solomon Mndeme amempongeza Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Shinyanga No. Hilda Boniphace kwa kazi nzuri anayoifanya yeye na wasaidizi wake ya kuinua Ushirika katika Mkoa wa Shinyanga na kwamba Serikali ya Mkoa wa Shinyanga itampatia ushirikiano wakati wote huku.

Mhe. Mndeme ameyasema hayo katika Hafla ya kufunga Programu ya Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani (SUD 2023) Mkoani Tabora ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein M. Bashe (MB) huku akitoa taarifa ya Mkoa wa Shinyanga kupokea Tzs. Bilioni 11.1 kwa ajili ya ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji Kata ya Nyida Shinyanga (V), kupokea mbolea Tani elfu 5, mahindi kupitia NFRA tani 2760, kuuza tumbaku kilo milioni 11.8 kwa wastani wa Dola 2.3 na kufikia Juni 2, 2023 imeuza Pamba kilo Milioni 3.9 na ununuzi unaendelea huku ikitenga Hekari 920 kuwapatia vijana wa BBT Wilayani Ushetu.

"Katika kutekeleza dhana hii ya Ushirika, nina wiwa kumpongeza sana Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniphace na wasaidizi wake kwa kujituma katika kazi kuinua ushirika Mkoani Shinyanga jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni anafanya kazi nzuri, nasi tutampatia ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza kazi zake kwa ufanisi zaidi," alisema Mhe. Mndeme.

Naye Waziri wa Kilimo Mhe. Bashe aliwaeleza wana Ushirika, viongozi wa Serikali, dini na wananchi waliohudhuria maadhimisho kuwa Serikali itaendelea kuwawezesha wana Ushirika katika kuboresha utoaji wa pembejeo ikiwamo mbolea, dawa za mimea, vitendea kazi. Aidha Mhe. Bashe kupitia hadhara hii ametoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Wilaya Nchini kuorodhesha vijana wote wenye maeneo makubwa ya kilimo ili Serikali iwawawezeshe kupitia Ofisi hizo katika nyenzo, pembejeo lengo ni kuimarisha sektaya kilimo kwa vijana nchini.

Kwa upande wake Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Shinyanga Bi. Hilda Boniface aliishukuru sana Serikali ya awamu ya sita inayoongwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo kwa nia yake ya dhati kabisaap ambapo kupitia Wizara ya kilimo imelenga kuimariaha Ushirika Nchini kwa kuimariaha usimamizi na udhibiti.

Lakini pia Serikali imempigania mkulima kwa kutoa ruzuku kwenye pembejeo na madawa ya kilimo na pia Wizara kupitia Tume ya Maendeleo ya ushirika Nchini imeendelea kuweka mipango ya usimamizi wa vyama hivi kwa kuanzisha mfumo wa Tehama wa Usimamizi wa vyama hivi unaitwa MUVU.

Bi. Hilda alisema kuwa Serikali imeleta mizani za kidigitali ili kulinda mazao ya mkulima na mwanaushirika, imeendelea kuongeza vitendea kazi muhimu kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa ushirika Mkoani kwetu na sasa tunaweza kujionea katika wiki hili la ushirika hapa Mkoani Tabora.

"Mimi kama Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Shinyanga ninae msaidia kazi Mrajis wa Vyama vya ushirika Nchini, na amabye Msimamizi ngazi ya Mkoa kwa kushirikiana na viongozi wangu wa Serikali ya Mkoa katika kuunga mkono jitihada hizi ambazo zinafanywa na Serikali chini ya Mhe. Waziri wa kilimo nitahakikisha ninafanya kazi yangu ya usimamizi kwa weledi mkubwa ili kuhakikisha ushirika wetu unaimarika, kurudisha heshma ya ushirika kwa kuhakikisha vyama hivi vinatekeleza madhumuni ya kuanzishwa kwake kwa kuzingatia sheria , kanuni na miongozo mbalimbali inayotolewa na TCDC," alisema Hilda.

Hilda alisema katika kulitekeleza hili tunahitaji zaidi viongozi wa ushirika wenye nia njema na vyama hivi ambao kupitia kazi zao watasaidia wanaushirika na wananchi wengine walio nje ya ushirika kutamani kujiunga na ushirika kutokana na huduma mbalimbali ambazo wao kama viongozi wanapaswa kuwahudumia wanachama wake ili lengo la kuinua uchumi wa mwanachama mmoja mmoja liweze kuonekana.

Ninazidi kuhamasisha wananchi mbalimbali wenye shughuli za kiuchumi waweze kujiunga na ushirika ili kupitia umoja wao wataweza kuyatatua matatizo ya kiuchumi na kijamii yanayowakabili kwani ushirika ndio nyenzo pekee ya kuimariaha uchumi kwa wenye kipato cha chini.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa