• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Mradi wa Usichana wangu kwanza watambulishwa Mkoani Shinyanga

Posted on: April 20th, 2017

Asasi ya kitaifa ya “Thubutu Africa Initiative” imetambulisha mradi wa kuwasaidia wasichana waliopevuka kupata kwa urahisi pedi za bei nafuu ili ziwasaidie kipindi cha hedhi.

Akizungumza wakati wakutambulisha mradi huo, ambao utaanza kwa majaribio Mkoani hapo kwa miezi mitatu, Mkurugenzi Mtendaji wa mradi Bw. Jonathan Kifunda amesema changamoto kubwa iliyopo katika jamii nyingi ni kuwa, wazazi hawazungumzi na watoto wa kike kuhusu hedhi matokeo yake watoto wengi wanaingia kwenye hedhi bila taarifa, hivyo wanakutana na madhara mengi ikiwemo kuchekwa na wenzao mashuleni hatimaye wanashindwa kujiamini hata kuogopa shule.

Bw. Kifunda amesema kutokana na utafiti uliofanywa na shirika la SNV kanda ya ziwa mwaka 2014, asilimia 82 ya watoto wa kike wanaingia kwenye hedhi bila kujitambua, wakati asilimia 70 ya utoro mashuleni unasababishwa na wanafunzi wa kike kushindwa kuhudhuria masomo siku za hedhi.

Amesema pia kuwa, wazazi asilimia 60 hawazungumzi na watoto wao kuhusu hedhi lakini wako tayari kuwaunga mkono watoto wao iwapo pedi za bei nafuu zitapatikana ili waweze kuwanunulia.

“Kama suala la hedhi ni la kuficha, sisi tunafunguka” amesema Kifunda.

Mkurugenzi huyo amesema mradi huo utatoa elimu kwa watoto wa kike mashuleni kwa kuomba muda maalumu wa kuwafundisha wasichana wanaotarajia na ambao tayari wamepevuka, kwa wazazi ili waweze kuzungumza na watoto wao pamoja na kusambaza pedi za bei nafuu kupitia wajasiriamali watakaofundishwa ili kila msichana aweze kumudu kuzipata.

Akieleza madhara ya kutozungumzia suala la hedhi, Bw. Kifunda amesema kuwa, wasichana wamekuwa wakipata shida wanapokuwa katika siku za hedhi na kwa sababu hakuna mawasiliano katika hilo wanajikuta wakitumia karatasi, majani ya miti, pamba n.k katika kujisitiri hivyo kusababisha magonjwa ya kansa na ugumba.

Amesema kwa kipindi cha miezi mitatu ya majaribio ya awali ya mradi lengo ni kufikia shule 6, watoto wa kike 700, wazazi 600 na wajasiriamali wanawake wanne watakaosambaza pedi za bei nafuu katika Wilaya za Kishapu na Shinyanga.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu Bw. George Andrea kwa niaba ya Serikali ya Mkoa, ameishukuru “Thubutu Africa Initiative” kwa kubuni mradi huo ambao amesema utawanufaisha watoto wengi wa kike na kuwa Serikali itakuwa bega kwa bega na wadau hao katika kufanikisha adhma ya kusaidia watoto wa kike Mkoani Shinyanga.

Naye Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bw. Mohamed Kahundi amekiri kuwa ni kweli utoro mashuleni bado ni changamoto na tatizo kubwa kwa watoto wa kike ni hedhi.

Hivyo amewasisitiza wadau hao kutimiza lengo la kusaidia watoto wa kike ili wasome katika mazingira bora na kuinua elimu yao bila kubadili nia na mipango ya Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUOMBA NAFASI YA UJUMBE WA BODI YA HOSPITALI YA MKOA January 03, 2020
  • Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha nne 2019 January 09, 2020
  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa Kidato cha pili 2019 January 09, 2020
  • Mwenge wa Uhuru kuwasili Mkoani Shinyanga May 07, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU 100

    June 27, 2021
  • SIKU MIA 100 ZA RAIS SAMIA

    June 27, 2021
  • DKT. SENGATI AHAIDI KUPAMBANA NA CHANGAMOTO YA UMASIKINI SHINYANGA

    June 05, 2021
  • Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga aapishwa

    June 02, 2021
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa