• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MTOTO AKIMJUA MUNGU ITAPUNGUZA MMOMONYOKO WA MAADILI - RC MACHA

Posted on: June 1st, 2024

Na. Paul Kasembo, KAHAMA.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amesema kuwa mtoto akimjua Mwenyezi Mungu itasaidia sana kupunguza mmomonyoko wa maadili kwani watakuwa wameishi na kutenda yale yote yanayoelekezwa na dini zetu ambayo kimsingi ndiyo mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwetu sote na ndiyo maadili ya Kitanzania huku akipongeza kwa mkutano mkubwa wenye hadhi ya Kimataifa.

RC Macha ameyasema haya leo katika hitimisho la Mkutano wa Waadventisti Wasabato Ukanda wa Dhahabu wenye hadhi ya Kimataifa uliofanyika Kanisa la Sabato Nyahanga Wilayani Kahama mkutano uliopewa jina la "KAHAMA NET EVENT 2024, YATOSHA JANGWANI" na kushuhudiwa na maelfu ya watu ndani na nje ya nchi kupitia vyombo mbalimbali vya habari na kutafsiriwa kwa lugha ya Kinyarwanda, Kifaransa, Kiingereza na Kiarabu.

"Pamoja na pongezi nyingi kwa kuandaa mkutano huu wenye hadhi ya Kimataifa, lakini kubwa zaidi niseme tu kwamba Watoto wetu wakilelewa katika misingi ya kumjua Mwenyezi Mungu hakika itapunguza sana mmomonyoko wa maadili katika jamii," amesema RC Macha.

Katika hotuba yake pia amepongeza kwa umahiri mkubwa uliotumika kuandaa mkutano huu mkubwa wenye hadhi ya Kimataifa ambao umerushwa kwa lugha yetu ya Kiswahili na hivyo kuitangaza lugha yetu na nchi Kimataifa kutokea Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga, huku akisisitiza kuwa jambo hili limeipatia heshima kubwa lugha na nchi yetu na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na madhehebu yote likiwemo la Wasabato.

Kwa upande wa risala iliyosomwa kwa niaba ya uongozi wa Kanisa imesema kuwa mkutano huu ulioanza rasmi tarehe 11 Mei, 2024 umeweza kutoa mafundisho mbalimbali ikiwemo Malezi ya watoto na familia, ujasiliamali, afya na afya ya akili umehitimishwa leo tarehe 1 Juni, 2024 huku kanisa likitoa ombi maalum la kupatiwa eneo litakaloweza kujengwa Kituo cha Vivutio na nyumba za watumishi wa Kanisa hapa Kahama jambo ambalo RC Macha amelipokea na kuridhia.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa