Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU 2023 WAPITISHA MIRADI YOTE 6 WILAYANI KISHAPU

Posted on: July 27th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MBIO za Mwenge wa Uhuru 2023 zimezindua, kukagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi 6 yenye thamani ya Tzs. 1, 369, 454, 000/= katika Wilaya ya Kishapu ikiwamo barabara ya Buganika - Kabila KM 11, thamani ya Tzs. 250, 000, 000/ kuzindua madarasa 02 ya awali na kupanda miti 300- Idukilo thamani yake  Tzs. 55, 824, 000/ kutoka Serikali Kuu na Tzs. 4,300,000 kutoka kwa wananchi, kuzindua jengo la wazazi, upasuaji na kulia nguo Kituo cha Afya Nelegani lenye thamani ya Tzs. 400, 000, 000/ kutoka Serikali Kuu na Tzs. 17,000,000/ kutoka Halmashauri

Miradi  mingine ilikuwa ni kuzindua mradi wa maji Masagala uliopo Maganzo, kukagua shughuli za utunzaji wa mazingira pamoja na upandaji wa miti katika Bwawa la Songwa 2, 330, 000/ pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi vyumba vya 42 vya biashara vyenye jumla ya Tzs. 240,000,000/ zitokanazo na mrejesho wa gawiwo la sehemu ya faida (CSR) na kwamba jumla ya thamani kwa miradi yote ni Tzs. 1, 369, 454, 000.00

Pamoja na kasoro zilizojitokeza katika mradi wa ujenzi wa Kituo vha Afya Nelegani, lakini kwa ujumla wake miradi imepongezwa sana kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 kitaifa Ndg. Abdalla Shaib Kaim huku akiwataka kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza katika mradi huo.

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mradi wa Maji kijiji cha Masagala Kata ya Maganzo Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo aliwashukuru sana viongozi wa Mwenge kwa kufika eneo hilo na kuzindua huku akisema kuwa uwepo wa mradi huo unakwenda kuwanufaisha wananchi wa kijiji cha Masagala na maeneo jirani.

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini - RUWASA Kishapu wametekeleza upanuzi wa mradi huo wa maji ambao chqnzo chake kikuu ni maji ya Ziwa Victoria chanzo chake ni Bomba la KASHWASA na umetekelezwa kwa kutumia mafundi wa ndani kwa gharama ya Tza. 399, 761, 591/.

"Ndugu zangu,  mradi huu wenye tangi moja kubwa lenye ujazo wa lita 100,000 linaweza kuhifadhi maji ambauo yatatumika kwa wananchi 94, taasisi 2 na biashara 3. Na kwamba mtandao huu wa maji wenye jumla ya kikomita 28.91 za bomba, mtandao wa bomba wa zamani kilomita 17.11 na mtandao mpya ni kilomita 11.80 unakwenda kupunguza kabisa kama siyo kuondoa tatizo la maji katika maeneo haya ya Masagala na vijiji jirani," alisema Mhe. Butondo.

Mwenge wa Uhuru unaendelea tarehe 28 Julai, 2023 katika Wilaya ya Shinyanga kwwnye Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ambapo utatembele miradi 10 ya maendeleo.

Picha ikionesha sehemu ndogo ya muonekano wa vyumba 42 vya biashara stendi ya mabasi Maganzo

Vyumba 02 shule ya awali vikikaguliwa

Ufunguzi wa Kituo cha Afya Nelegani

Uzinduzi wa mradi wa maji kijiji cha Masagala Kata ya Maganzo

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa