• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Shinyanga yazindua rasmi dawati la malalamiko

Posted on: September 30th, 2017

Ofisi ya Rais TAMISEMI na Ofisi ya Rais UTUMISHI kwa kushirikiana na Mradi wa uimarishaji wa mifumo ya Sekta ya Umma nchini PS3 wamezindua mfumo wa dawati la malalamiko katika ngazi ya Mkoa kwa lengo la kutekeleza dhana ya utawala bora.

Uzinduzi huo umefanyika mwishoni mwa wiki hii katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuhudhuriwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa bw. Burton Mwakanyamale, Maafisa Utumishi na Utawala Ofisi ya Rais TAMISEMI na UTUMISHI, Meneja Mradi wa PS3 Mkoa, Bi. Joyce Mfinanga, Mratibu wa PS3 Sekretarieti ya Mkoa, Wakuu wa Sehemu na Vitengo pamoja na baadhi ya watendaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mfumo huo utawawezesha wananchi kulalamika kwa njia rahisi zaidi, kwani kutakuwa na Ofisi maalumu ya Malalamiko itakayokuwa na Afisa mahsusi wa kupokea malalamiko yote, fomu maalumu za malalamiko zitakazopatikana katika tovuti ya Mkoa na tovuti za Halmashauri ambayo wananchi wataipakuwa na kujaza kisha kuiwasilisha ofisini, Aidha, kutakuwa na simu ambayo wananchi watapiga kuwasilisha malalamiko yao.

Mshauri wa masuala ya Utawala bora wa Mradi wa PS3 Dkt. Nazar Sola amesema katika Sera utawala bora, kuwawezesha wananchi kutoa malalamiko ni mojawapo ya uimarishaji wa Sera hiyo muhimu kwani inasaidia kutatua matatizo na kero za wananchi katika ngazi za awali na mapema zaidi.

Dkt. Nazar amesema mfumo huu wa malalamiko ambao utamilikiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI, umeanzishwa katika mikoa minne ya Kigoma, Dodoma, Mtwara na Shinyanga. Amesema, kwa Mkoa wa Shinyanga mfumo unafanyiwa majaribio katika wilaya ya Kishapu na tayari umeshazinduliwa kwa kuanzisha ofisi au madawati ya malalamiko katika ngazi ya Halmashauri, Kata, vijiji, vituo vya afya, zahanati, Hospitali, shule ya msingi na Sekondari.

Naye Afisa Utumishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Neema Nguku amesema mfumo wa dawati la malalamiko umekuja kutokana na mapungufu yaliyoonekana katika utaratibu wa maboksi ya maoni uliokuwepo ambapo ilibainika kuwa hayakutumika kikamilifu. Bi Neema amesema,baada ya mapungufu hayo Katibu Mkuu TAMISEMI alitoa maelekezo ya watumishi kuvaa beji wawapo kazini ili wananchi wapate nafasi ya kulalamika dhidi ya watumishi wasio waadilifu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa