• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AHIMIZA UJENZI WA NYUMBA BORA USHETU

Posted on: April 20th, 2024

Na. Paul Kasembo - USHETU.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha ametembea katika Kata Igwamanoni iliyopo Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama ili kuwajulia hali waathirika wa mvua pamoja na kuhimiza ujenzi wa nyumba bora zenye kuanza na msingi wa mawe, tofali za kuchoma au za saruji ili kukabiliana na athari zitokanazo na mvua zinazoendelea.

Haya yametolewa leo tarehe 20 Aprili, 2024 ambapo RC Macha awali alitaarifiwa kuwa zaidi ya  nyumba mia tano (500) zimeathirika na mvua huku kaya 21 zikiwa zimekosa kabisa makazi ya kuishi ambapo athari hizi imetajwa kutokea katika nyakati tofauti tofauti huku tarehe 10 Aprili, 2024 ndiyo kunatajwa kuwa nyumba nyingi zaidi ziliathirika zaidi na hivyo kufika idadi hii.

Pamoja na kuwashukuru sana ndugu na jamaa wote waliojitolea kuwahifadhi wahanga wa mvua hizi, RC Macha amesema kuwa, Serikali haitawaacha wapate shida na hivyo amemuagiza DC wa Wilaya ya Kahama kufanya tathimini ya amhao bado hawajapata usaidizi wa aina yoyote ili waone namna ya kuwasaidia.

"Tumekuja kuwapa pole nyote mlioathirika na mvua hizi zinazoendelea hivi sasa pamoja na kuwapa salamu za Serikali kuwa ipo nanyi wakati wote, lakini pia kuwataka nanyi muanze ujenzi wa nyumba bora zenye kuanza na msingi wa mawe chini, tofali walau za kuchoma na hasa ziwe za saruji ili kuweza kukabiliana na janga la aina yoyote ikiwemp maafa yatokanayo na mvua nyingi," amesema RC Macha.

Awali akitoa taarifa ya uwepo wa maafa yatokanayo na mvua hizi, Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita amesema kuwa, katika athari hizi Kata ya Igwamanoni iliyopo Ushetu ni moja kati ya maeneo ambayo wananchi wake wameathirika sana na mvua hizi, ambapo pamoja na kupoteza baadhi ya makazi lakini pia miundombinu ya barabara imeharibika zaidi hasa kati ya Igwamanoni na Kata ya Luhaga iliyopo mpakani mwa Mbogwe - Geita.

Kando na maelekezo haya, pia RC Macha ametoa siku 4 kwa TARURA Wilaya ya Kahama kuhakikisha kuwa wanarekebisha na kurejesha mawasiliano ya haraka kupitia baarabara ya Igwamanoni hadi Luhaga ambayo imeathirika zaidi jambo ambalo linapelekea kukatika kwa mawasiliano kabisa ili wananchi waendelee kupata huduma.


HABARI PICHA



Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa