• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AISHAURI JAMII YA SHINYANGA KUPIMA AFYA MARA KWA MARA

Posted on: June 18th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha, amewashauri wananchi mkoani Shinyanga kujenga utamaduni wa kupima Afya zao mara kwa mara, huku akimpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha huduma za Afya nchini.

RC Macha amebainisha haya leo Juni 18, 2024 wakati alipotembelea kuona Maendeleo ya ujenzi wa uboreshaji wa Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga, pamoja na utoaji huduma za Afya kutoka kwa Madaktari Bingwa wa Rais Dkt. Samia ambao wanaendelea na utoaji wa matibabu ya kibingwa kwa wananchi wa hapa mkoa wa Shinyanga.

Amesema wananchi wengi wamekuwa wakisumbuliwa na Magonjwa na kufikia katika hatua mbaya, hali ambayo inasababishwa na kutopima Afya mara kwa mara, ili kupata ushauri wa Daktari kwa kulinda Afya au kuanza Tiba mapema.

“Wananchi nimeona mmejitokeza kwa wingi kuja kupata Matibabu kutoka kwa Madaktari Bingwa wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hivyo natoa wito kwa wananchi wa Shinyanga mjenge tabia ya kuchunguza Afya zenu mkiwa bado wazima na siyo kusubili hadi mnakuwa katika hali mbaya,”amesema Macha.

“Mkipima Afya zenu mapema itawasaidia kujua hali zenu, na ukibainika unatatizo unaanaza matibabu mapema na kupona, Mfano Magonjwa haya ya Saratani ya Matiti na Shingo ya kizazi ukiwahi matibabu mapema unaweza kupona kabisa,”ameongeza Macha.

Aidha, amesema katika Shinyanga watapanga namna ya kuweka utaratibu wa wananchi wawe wanapima afya zao mara kwa mara, huku, akiwataka pia wananchi wakate Kadi za Bima za Afya ambazo zitawasaidia kupata matibabu kwa urahisi bila ya kuingia gharama kubwa na kuokoa Afya zao.

Katika hatua nyingine amempongeza Rais Samia kwa kutoa fedha na kuboresha huduma za Afya nchini, ikiwamo na Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga, ambayo kwa sasa ujenzi wake unakwenda kukamilika kwa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD), najengo ya upasuaji na Wodi.

Naye Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga Dk. Elisha Robert amesema ujenzi wa uboreshaji wa Hospitali hiyo ya Manispaa ya Shinyanga utakamilika Juni 30, 2024.

Nao baadhi ya wananchi wa Shinyanga, wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za Afya, huku wakiwaletea pia Madaktari Bingwa na kuwapatia Matibabu ya Kibingwa na kuimarisha Afya zao.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa