• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AKABIDHI GARI JIPYA KWA RUWASA MKOA WA SHINYANGA

Posted on: October 28th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amemkabidhi gari jipya STN 2943 Mhandisi Julieth Payovela ambaye ni Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Shinyanga katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga huku akisisitiza kuwa ikatumike kwa kadiri ya lengo kusudiwa la serikali.

Hafla hii imefanyika leo tarehe 28 Oktoba, 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude, pamoja na watumishi mbalimbali kutoka RUWASA na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwezesha watumishi kutekeleza kazi zao kwa ufanisi zaidi na kuwahudumia wananchi kwa wakati na kuwafikia kwa haraka zaidi.

"Kwanza tumshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwawezesha watumishi katika Wizara, Sekta na Ofisi zake zote ili kurahisisha utekelezaji na usimamizi wa shughuli za kila siku kama ambavyo imefanyika kwa wenzetu hawa RUWASA Mkoa wa Shinyanga, niwaombe kwenda kutumia gari hili kwa kadiri ya lengo lililokusudiwa na Serikali na wala isiwe vinginevyo," amesema RC Macha.

Kando na hayo, ameitaka RUWASA Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha kuwa gari hili linatunzwa kwa maslahi mapana ya Serikali ili lidumu muda mrefu na lifanyiwe matengenezo stahiki pale inapohitajika kufanya hivyo huku akiwataarifu waalikwa wa hafla hii kuwa anatambua, anathamini na kuheshimu zaidi kazi, ubunifu, weledi na utendaji kazi wa Meneja RUWASA Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Julieth.

Kwa upande wake Mha. Julieth amemshukuru sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha ofisi yake kupata kitendea kazi ambacho kinakwenda kuongeza ufanisi na uboreshaji wa utekelezaji wa majukumu ya kila siku, huku akimpongeza RC Macha kwa kuendelea kuisaidia RUWASA katika utekelezaji wa kazi zake mkoani Shinyanga.

Upokeaji wa gari hili jipya STN 2943 kwa RUWASA Shinyanga unakwenda kurahisisha usimamizi na ufuatiliaji wa miradi wa miradi yake.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa