• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AKABIDHI TREKTA ZA MIKONO 12 ZILIZOTOLEWA NA NBC BENKI - SHINYANGA

Posted on: November 16th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amekabidhi vifaa vya kilimo (Trekta za Mikono 12 ) zilizotolewa na Benki ya NBC Tawi la Shinyanga ambazo wamekabidhiwa wakulima 12 kutoka Kata ya Masengwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga huku akiwashukuru na kuwapongeza sana Benki ya NBC kwa ubunifu wao huu wa kukopesha wakulima tena wa kawaida kabisa kwa vigezo rahisi na rafiki sana.

RC Macha amekabidhi na kusisitiza hayo tarehe 16 Novemba, 2024 katika hafla fupi iliyofanyika mbele ya jengo la NBC Benki tukio ambalo liliratibiwa, kusimamiwa na kutekelezwa vema na Meneja wa Tawi hili Bi. Joyce Chagonja na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Wakili, Julius Mtatiro.

Wengine waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ndg. Edward Ngelela, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Ngassa Mboje, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ndg. David Rwazo, wakulima na watumishi wa NBC Bank na wananchi ambapo amewataka wakulima kwenda kujiorodhesha katika maeneo yao ili waweze kutambulika na kuwa rahisi kunufaika pindi fursa zinapojitokeza.

"Kwa dhati kabisa nawapongeza sana Benki ya NBC Tawi la Shinyanga kupitia kwa Meneja wake Bi. Joyce Chagonja kwa muendelezo huu wa kutoa mikopo ya vifaa vya kilimo kwa wakulima wetu hasa hawa wa kawaida kabisa, hakika mmedhihirisha kuwa inawezekana kwa mkulima kupata mkopo huu tena kwa vigezo rahisi na rafiki ambavyo mkulima yeyote anawezamudu kuwa navyo, hongereni sana," amesema RC Macha.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NBC Tawi Bi. Joyce amesema kuwa baadhi ya vigezo ni mkulima kuwa na shamba, kutambulika na uongozi wa kitongoji/kijiji, anayetumia mifumo ya kibenki katika kuuza mazao yake, awe mkulima wa zaidi ya miaka mitatu au zaidi, shamba lenye ukubwa wa hekari 10 au zaidi, awe anatambulika na Chama cha Ushirika huku akisisitiza kuwa huu ni mwendelezo wa mikopo ya vifaa vya kilimo lengo ni kuwawezesha kuwa na kilimo cha kisasa na chenye tija zaidi kwao.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa