• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA APIGA KURA MTAA WA LUBAGA FARM

Posted on: November 27th, 2024

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha mapema leo tarehe 27 Novemba, amefika Kituo cha Kupiga Kura kilichopo Mtaa wa Lubaga Farm hapa Manispaa ya Shinyanga na kupiga kura kutimiza haki hake ya Kikatiba huku akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kupiga kura na kurudi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali ambapo baadae watatangaziwa matoke.

RC Macha ametoa wito huu leo ikiwa ni siku maalum ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo wananchi wamepata nafasi ya kuchagua Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji, Vitongoji, pamoja na wajumbe, wao ambao watawatumikia wananchi kwa kipindi cha miaka mitano hadi 2029.

"Leo hii ndiyo siku pekee ambayo tumekuwa tukiisubiria sana ambapo kila mwananchi aliyejiandikisha, mwenye vigezo anapaswa kupiga kura kuwachagua viongozi wetu ambao watahudumu kwa miaka mitano kuanzia leo, hivyo niwakumbushe wananchi kutumia muda kwenda kupiga kura na kisha kuendelea na shughuli zetu za kila siku na matokeo watatangaziwa," amesema RC Macha.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Kanda ya Serengeti ndg. Jackson Mnyawami ambaye naye alifika hapa kupiga kura amesema kuwa zoezi la Uchaguzi katika kituo hiki lipo vizuri na linakwenda salama huku akiomba maboresho kwa baadhi ya vituo huku akitoa wito kwa wanachama na wananchi kujitokeza kutumia haki yao muhimu ya Kikatiba ili kuwapata viongozi wao.

Katika Kituo hiki cha Lubaga Farm, pamoja na wananchi mbalimbali kufika hapa Kupiga Kura lakini pia amefika Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni, Katibu wa CHADEMA Kanda ya Serengeti ndg. Jackson Mnyawami ambao wote kwa nyakati tofauti wametimiza takwa la Kikatiba la kuchagua viongozi wao.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Mkoa wa Shinyanga unajumuisha Mitaa 130, Vijiji 506, Vitongoji 2704 na utakuwa na Vituo vya Kupiga Kura 3080.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa