• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA APOKEA VIFAA TIBA

Posted on: June 5th, 2024

Na. Paul Kasembo, KISHAPU.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amepokea Vifaa Tiba kutoka NMB Kanda ya Magharibi vyenye thamani ya zaidi ya Mil. 24 kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Kishapu, Kituo cha Afya Ngw'anharanga na Zahanati ya Busongo vifaa ambavyo vimekabidhiwa na Ndg. Seke Urio ambaye ni Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi huku akisisitiza juu ya kutambua, kuthamini na kuheshimu kazi njema zinazofanywa na NMB Benki.

RC Macha katika salamu zake kwa NMB pamoja na kuwapongeza sana lakini pia amewataka kutoridhika na kubweteka kwakuwa wamekuwa na mafanikio makubwa zaidi na badala yake waendelee na kasi hii waliyonayo hivi sasa ili waweze kufikia malengo makubwa zaidi ambayo yatawanufaisha wananchi walio wengi na ambao ndiyo walengwa hasa, kupata faida wao, kulipa kodi na kutoa mrejesho  wa 0.01% (CSR) itokanayo na faida baada ya kulipa Kodi ya Serikali.

"Kwa dhati kabisa nawapongeza sana NMB Benki kwa kazi nzuri mnazozifanya kwa wananchi ikiwemo kutoa mrejesho kwa jamii katika Sekta ya Afya, Elimu nk ambapo leo kwa niaba ya Serikali na wananchi nimokea kutoka kwenu vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Mil. 24 hongereni sana NMB," amesema RC Macha.

Aidha RC Macha amesema kuwa, kwa wale wote ambao wamekuwa wakikutana na kadhia ya Mikopo inayoathiri vipato vyao kutokana na riba kuwa kubwa (Kausha Damu), ni wakati sasa umefika wa kuachana na mikopo hiyo na badala yake watumie Taasisi za fedha (Benki) ikiwemo NMB kupata mikopo ambayo haitatweza na kuondoa utu wao machoni mwa jamii na yenye staha huku akitaja "MSHIKO FASTA" ni suluhisho la Kausha Damu iwapo tu mkopaji atakuwa amekidhi Shetia, Kanuni na Masharti ya Benki.

Pamoja na pongezi, pia amewataka watumishi na watoa huduma wilayani Kishapu kuhakikisha kuwa vifaa tiba hivi vilivyotolewa vinatunzwa na kutekeleza kazi iliyokusudiwa na wala siyo vinginevyo.

Awali akitoa salamu za NMB Ndg. Urio amesema kuwa kwa Benki yao imejidhatiti sana katika uboreshaji wa utoaji wa huduma ambapo Wilaya zote nchini kwa asilimia 100 na kwamba uchangiaji wa CSR kwa jamii ni utaratibu wa kawaida kwa kila mwaka.


HABARI PICHA


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa