• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AWATAKA WANAFUNZI WA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA SEKONDARI KUSOMA KWA BIDII

Posted on: September 18th, 2024

Na Paul Kasembo, SHY RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamiringi Macha amewaasa wanafunzi wa Shule ya Wasichana Shinyanga Sekondari kuweka jitihada na nguvu zote katika masomo ili kuhakikisha wanafanya vizuri na baadae waweze kutimiza ndoto na malengo waliyojiwekea ukizingatia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha kila kitu ikiwemo kuleta walimu, kujenga shule, kuweka miundombinu yote muhimu, kuleta vitabu, nishati ya umeme, maji na vingine vingi iliyobakia ni ninyi kusoma kwa bidii na ndiyo shukrani zenu pekee kwake Mhe. Rais.

Ameyazungumza hayo leo tarehe 18 Septemba 2024 alipotembelea shule hii akiwa ameambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Salum Hamduni, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Masumbuko, Katibu Tawala Wilaya ya Shinyanga ndg. Said Kitinga, Mkurugenzi wa Manispaa Mwl. Alexius Kagunze na watalaam wengine.

Pamoja na ushauri huu, pia RC Macha ameipongeza sana Manispaa ya Shinyanga kwa usimamizi wa ujenzi wa shule hii ambayo inatajwa kuwa ya mfano kutokana na ubora, thamani yake pamoja na uahirikiano wao mzuri jambo ambalo linapelekea kukamilika kwa ujenzi huu ifikapo mwishoni mwa Septemba 2024.

“Ninawataka na kuwatia moyo sana ninyi wanafunzi wote katika shule hii, muelekeze bidii na jitihada zenu kubwa katika masomo yenu ili muhakikishe kwamba mnafanya vizuri na mnakuwa mfano wa kuigwa kwa wanafunzi wengine ambao watafuata baada yenu na pia kwa wanafunzi wa shule zingine na hatimaye muweze kuzifikia, kutimiza na kuziishi ndoto zenu pamoja na malengo mliyojiwekea ukizingatia Mhe. Rais wetu mpendwa amekwishaleta na kuwezesha kila kitu hapa” amesema RC Macha.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga CP. Hamduni amewataka watumishi wa Serikali mkoani Shinyanga kuwa makini katika kutekeleza kazi za Serikali, kutanguliza uzalendo na kuhakikisha kuwa thamani ya fedha inaonekana kwenye kazi zote na hasa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili iwe na tija iliyokusudiwa huku akisisitiza kwenda na kasi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwahudumia na kuwaletea maendeleo wananchi wetu.

Akipokea ushauri huo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Mwl. Kagunze ameahidi kutekeleza kazi kwa viwango na kwa wakati ili kwenda na muda uliokusudiwa ambapo ujenzi wa shule hii unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Septemba 2024. 

Aidha Kagunze ameongeza kuwa kufikia Januari 2025 Shule ya Wasichana Shinyanga Sekondari itakuwa tayari kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza ambao watakuwa wamechaguliwa hapo kwa kuwa miundombinu yote ya shule ipo tayari.

Kukamilika ujenzi wa Shule ya Wasichana Shinyanga Sekondari kunatajwa kusadia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha wanafunzi wa Mkoa wa Shinyanga na Mikoa mingine kuwa na mazingira rafiki, mazuri na yenye kuvutia kwa kujisomea wanafunzi na kufundishia walimu kutokana na miundombinu bora iliyopo na kwamba hata thamani ya ardhi inaongezeka kutokana na uwepo wa shule hii.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa