• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AZINDUA WIKI YA MAADHIMISHO YA MEI MOSI, AWATAKA WAAJIRI KUWARUHUSU WAFANYAKAZI KUSHIRIKI

Posted on: May 1st, 2025

Na. Paul Kasembo, SHY RS.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha amezindua rasmi wiki ya maadhimisho kuelekea kilele cha Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei 1, 2025, hulu akitoa wito kwa waajiri wote mkoani Shinyanga kuwaruhusu wafanyakazi wao kushiriki kikamilifu kwenye maadhimisho haye.

Akizungumza Aprili 25, 2025 katika hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Uwanja wa Kambarage uliopo Manispaa ya Shinyanga, RC Macha amesema wiki ya wafanyakazi ni fursa ya kipekee kwa wafanyakazi kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii, zikiwemo huduma za afya na elimu, ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.

“Waajiri mnapaswa kuelewa kuwa ushiriki wa wafanyakazi katika maadhimisho haya siyo tu ni haki yao, bali ni njia mojawapo ya kuimarisha mshikamano, uhusiano na hivyo kuongeza morali kazini,” alisema RC Macha.

Aidha, RC Macha alisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa uhusiano mzuri kati ya waajiri na waajiriwa, akibainisha kuwa ushirikiano huo ni kichocheo kikubwa cha kuongeza tija na ufanisi katika maeneo ya kazi.

Katika hotuba yake, RC Macha alipongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi nchini.

“Rais wetu amekuwa akionesha dhamira ya dhati ya kuwapigania wafanyakazi. Tayari baadhi yao wamelipwa malimbikizo ya mishahara na wengine waliokuwa wamechelewa kupandishwa vyeo tayari wamepandishwa na wanaendelea kupata haki zao stahiki,” aliongeza RC Maxha.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Mkoa wa Shinyanga, Bw. Yohana Maremi, alisema kabla ya uzinduzi huo wanachama wa TUCTA walijitolea kufanya usafi katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga kama sehemu ya kuadhimisha wiki hiyo ya wafanyakazi.

Amesema jitihada hizo zimechangia kuboresha mazingira ya utoaji huduma hospitalini hapo na kuonesha mfano wa uwajibikaji wa kijamii kwa wafanyakazi.

Maadhimisho ya mwaka huu yamebebwa na kauli mbiu isemayo: "Uchaguzi Mkuu 2025, Utuletee viongozi wanaojali Haki na Maslahi ya Wafanyakazi, Sote Tushiriki".

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ENDELEENI KUTOA ELIMU ZAIDI KUHUSU AFYA YA AKILI - DC. MBONI

    May 30, 2025
  • TAKUKURU SHINYANGA YAANZA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA UBADHIRIFU WA SHILINGI MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU WA USHETU - DONASIAN.

    May 27, 2025
  • MAISHA BAADA YA KUSTAAFU YANAHITAJI UTULIVU - DC. MTATIRO

    May 26, 2025
  • MAFUNZO YA IPOSA NI MKOMBOZI KWA VIJANA WALIO WENGI WANAOKOSA FURSA YA ELIMU YA KAWAIDA - RC. MACHA

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa