• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AZITAKA HALMASHAURI MKOANI SHINYANGA KULIPA STAHIKI KWA WAKATI

Posted on: July 25th, 2024

Na. Paul Kasembo SHY RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amezitaka Halmashauri mkoani kuwalipa kwa wakati watoa huduma ya usafiri wa dharura ngazi ya jamii ili kuwawezesha kuendelea kutoa huduma wakati wote jambo ambalo litawaongezea tija zaidi ya kufanya kazi zaidi.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 25 Julai, 2024 wakati alipotembelea Banda Maalum la watoa huduma ya m-mama katika uwanja wa CCM Kambarage ambapo pamoja na mambo mengine amemshukuru na kumpongeza sana Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuifanya huduma hii inakuwa sehemu zote.

"Nizitake Halmashauri za hapa Shinyanga kuwalipa stahiki zao kwa wakati watoa huduma ya usafiri wa dharura ngazi ya jamii ili waendelee kutoa huduma kwa tija zaidi," amesema RC Macha.

Wakiongea kwa nyakati tofauti Dr. Yudas Ndungile (RMO) na  Bi Joyce (mtoa huduma m-mama) wamesema kuwa mgonjwa anapopiga simu 115 bure ataweza kufuatwa na huduma za usafiri wa gari (community tax) kutoka katika jamii ya eneo husika ambapo anapatikana na kupelekwa katika kituo cha afya kilichokaribu yake na kwa walio hospitali huchukuliwa na gari maalum la wagonjwa (ambulance).

m-mama ni utaratibu wa kuratibu na kutoa huduma ya usafiri wa dharura kwa mama mjamzito, mtoto mchanga na akina mama waliojifungua ndani ya siku 42 aliyepata shida kutoka sehemu aliyepo kwenda kituo kilicho karibu nae ili apate huduma anayostahili hata katika ngazi ya jamii mgonjwa.

Kwa upande wake Daktari kutoka Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga Dr. Abduel Mdee amesema kuwa kuna Kitita cha Uzazi Salama ambao ni mkusanhiko wa vitu vitatu ambayo ni mafunzo yanayoambatana na vifaa vya kutolea huduma na vya kujifunzia pamoja na matumizi ya takwimu ambazo zinakusanywa eneo la kazi lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa huduma ya mama mjamzito, kujifungua salama na mtoto anayezaliwa awe salama.

Huduma hii inapatikana Mikoa mitano ambayo ni Manyara, Tabora, Shinyanga, Geita na Mwanza na kwamba huduma hii imeazishwa miaka mitatu iliyopita kwa awamu ya kwanza na kuonesha mafanikio makubwa.


HABARI PICHA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha akiingia banda la m-mama

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dr. Yudas Ndungile akitoa maelezo mbele ya RC Macha

Picha ikiwaonesha watoa hudumu ya m-mama Mkoa wa Shinyanga

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa