• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MACHA AZITAKA HALMASHAURI MKOANI SHINYANGA KUWASHIRIKISHA WAZEE KATIKA VIKAO NA MIKUTANO YOTE.

Posted on: September 26th, 2024

Na. Paul Kasembo, USHETU.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amezitaka Halmashauri zote mkoani Shinyanga kuhakikisha zinawashirikisha na kuwaalika Baraza la Ushauri la Wazee katika maeneo yao ili waweze kushiriki katika vikao na mikutano yote ikiwa ni sehemu ya kutambua, kuwaenzi na kuthamini uwepo na mchango mkubwa katika Taifa hili.

RC Macha ameyasema haya leo tarehe 26 Septemba, 2024 alipoongoza Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani ambapo Kimkoa yamefanyika Kijiji cha Igunda kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa wazee akiwemo Makamu Mwenyekiti Baraza la Wazee Mkoa wa Shinyanga Mzee Richard Mihayo, Katibu wa Baraza Mkoa wa Shinyanga Mzee Anderson Lymo, Mbunge wa Jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani na wajumbe wote kutoka katika Halmashauri zote sita za Mkoa huku msisitizo zaidi ukiwekwa kwenye kujitunza, kujipenda na kushiriki shughuli za kijamii.

"Nitumie nafasi hii kuzitaka Halmashauri zote ndani ya Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha kuwa viongozi kutoka Baraza la Ushauri la Wazee wanashirikishwa kikamilifu katika vikao na mikutano yote katika maeneo yao ikiwemo katika Mabaraza ya Waheshimiwa Madiwani ili tuwaenzi, tutambue na kuthamini michango yao katika Taifa" amesema RC Macha.

Pamoja na kupokea risala ya wazee, RC Macha amewapongeza sana huku akiwakumbusha kuwa kuanzia tarehe 11 - 20 Oktoba, 2024 ni kipindi cha kujiandikisha katika daftari la wapiga kura, na itakapofika tarehe 27 Novemba, 2024 wajitokeze kupiga kura ili kuchagua viongozi ambao watakuwa na tija kwao ukizingatia kuwa wao ni wazee huku akihamasisha pia kugombea nafasi hizo kwani ni haki yao pia.

Kwa upande wake Mhe. Cherehani amesema kuwa, ofisi yake inatambua na kuthamini sana uwepo wa wazee katika Jimbo la Ushetu na kwamba yeye mwenyewe amekuwa akishirikiana nao wakati wote ambapo mpaka sasa amefanya mikutano takribani 272 katika vijiji vyote 112 na Kata 20 za Ushetu ambapo amekuwa akishirkiana nao vema huku akiwakumbusha mema mengi ambayo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameyafanya kwa Wanaushetu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAPITIO YA ROBO MWAKA KWA KIPINDI CHA OKT - DES 2024 CHA (PJT MMMAM) CHAFANYIKA MKOANI SHINYANGA.

    February 28, 2025
  • RCC SHINYANGA YARIDHIA MAPENDEKEZO NANE (8) YA MATUMIZI BORA YA ARDHI.

    February 27, 2025
  • KUKAMILISHWA KWA MIRADI YA BARABARA KUTAPUNGUZA KERO KWA WANANCHI – RC MACHA

    February 26, 2025
  • WALIMU, TOENI ELIMU INAYOENDANA NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA -RC MACHA

    February 24, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa