• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MBONI AKUTANA NA NDUGU WA WALIOFUKIWA NA MGODI, ATOA MAELEKEZO YA KUIMARISHA UOKOAJI.

Posted on: August 18th, 2025

 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, leo Agosti 18,2025 ametembelea eneo la tukio katika Mgodi wa Nyandolwa uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, na kukutana na ndugu wa wachimbaji waliokwama chini ya kifusi baada ya mgodi huo kutitia, ajali iliyohusisha mafundi takribani 25.

Katika mkutano huo, RC Mhita alitoa pole kwa familia na ndugu wa waathirika, akisisitiza kuwa serikali ya mkoa iko pamoja nao wakati huu mgumu na inaendelea kuchukua hatua zote za haraka kuhakikisha shughuli za uokoaji zinafanikiwa.

"Tunahitaji kila sekunde kuokoa maisha, juhudi zinaendelea usiku na mchana na tunawaombea wote waliopo chini ya kifusi wawe hai,” alisema RC Mhita.

Mhe. Mhita alibainisha kuwa Serikali tayari imeanza kutoa msaada wa chakula kwa wanafamilia walioko kwenye Mgodi huo wanaogojea kuokolewa kwa ndugu zao 18 ambao bado wamekwama chini ya kifusi ili kuwapa faraja wakati shughuli za uokoaji zikiendelea.

Kwa mujibu wa RC Mhita, hadi sasa watu 7 wameokolewa kutoka kwenye kifusi, ambapo kwa masikitiko makubwa, 4 kati yao wamethibitika kupoteza maisha, na wengine 3 wakiwa hai na wanaendelea kupatiwa huduma za matibabu. Hii inafanya idadi ya mafundi waliobaki chini ya kifusi kufikia 18.

 Mafundi hao walikuwa wakitekeleza kazi ya ukarabati wa mgodi unaomilikiwa na kikundi cha Mchapakazi, kwa ajili ya kuanza tena uzalishaji, kabla ya ajali hiyo kutokea na mgodi kutitia ghafla.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa