• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MBONI MHITA AIPONGEZA TISEZA, ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI SHINYANGA.

Posted on: July 4th, 2025

Sabasaba 2025.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, @mboni_mhita ametoa pongezi kwa Mamlaka ya Uwekezaji katika Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kwa juhudi na mafanikio wanayoendelea kuyapata katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini, hususan kwenye maeneo maalum ya kiuchumi.

Akizungumza alipofanya ziara kwenye banda la TISEZA katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayofanyika katika Viwanja vya J.K Nyerere, Barabara ya Kilwa – Dar es Salaam, Mhe. Mhita alisema kuwa TISEZA ni mfano wa Taasisi zinazotekeleza kikamilifu dhamira ya Serikali ya kuimarisha uchumi wa viwanda kupitia uwekezaji wa kimkakati.

"Napenda kuwapongeza TISEZA kwa kazi nzuri mnayoifanya. Mmekuwa sehemu muhimu ya kuhakikisha Tanzania inanufaika kikamilifu na fursa za kiuchumi zinazotokana na maeneo maalum ya uwekezaji," alisema Mhe. Mboni.

Katika mazungumzo yake na Maafisa wa TISEZA, RC Mboni alitumia fursa hiyo kuwakumbusha kuhusu uwepo wa maeneo kadhaa maalum ya uwekezaji mkoani Shinyanga. Alieleza kuwa Mkoa umejipanga vilivyo katika kutangaza fursa hizo kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, huku akisisitiza ushirikiano wa karibu na TISEZA katika kuzivutia rasilimali na mitaji ya maendeleo.

“Mkoa wa Shinyanga una ardhi kubwa, miundombinu inayoimarika, na nguvu kazi ya kutosha. Huu ni wakati wa kuhakikisha maeneo yetu maalum yanajulikana na kuvutia wawekezaji wa kweli,” aliongeza RC. Mboni.


Mazungumzo kati ya RC Mboni na uongozi wa TISEZA yamejikita zaidi katika njia bora za kuhamasisha uwekezaji na kukuza maendeleo ya kiuchumi mkoani Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya ajenda ya kitaifa ya kukuza viwanda, ajira, na kuongeza pato la taifa kupitia Sekta binafsi.


Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM APONGEZA USHIRIKI WA MKOA WA SHINYANGA KATIKA MAONESHO YA SABASABA.

    July 06, 2025
  • RC. MBONI ATOA WITO KWA TISEZA KUTANGAZA FURSA KUU YA KONGANI YA UWEKEZAJI BUZWAGI

    July 05, 2025
  • MHE. RIDHIWANI KIKWETE AWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA MKOA WA SHINYANGA KWENYE MAONESHO YA SABASABA

    July 05, 2025
  • KATIBU TAWALA WILAYA YA KAHAMA AWAPONGEZA WASHIRIKI WA MAONESHO YA SABASABA 2025 KUTOKA MKOA WA SHINYANGA

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa