• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MBONI MHITA APONGEZA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA KWA KUIMARISHA MAADILI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI.

Posted on: August 19th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ameipongeza Tume ya Utumishi wa Mahakama ya Tanzania kwa juhudi thabiti katika kusimamia na kuimarisha nidhamu, uwajibikaji na maadili miongoni mwa watumishi wa Mahakama nchini.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wajumbe wa Kamati za Maadili ya Maafisa wa Mahakama wa Mkoa wa Shinyanga na wilaya zake, Mhe. Mhita alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa kuwa yanawajengea uwezo wajumbe hao kutekeleza majukumu yao kwa weledi, haki na uadilifu.

“Mafunzo haya yana umuhimu mkubwa kwa sababu yanatoa fursa ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa Kamati za Maadili kutekeleza majukumu yao kwa haki na uadilifu. Tunatambua kuwa maadili bora ndiyo nguzo ya haki na msingi wa imani ya wananchi kwa chombo cha Mahakama,” alisema Mhita.

Aliongeza kuwa bila maadili thabiti, heshima na hadhi ya Mahakama hubakia mashakani, hivyo akasisitiza kuwa juhudi za Tume hiyo zinapaswa kuungwa mkono na wadau wote wa haki.

Aidha, RC Mhita alieleza kuwa Serikali ya Mkoa wa Shinyanga itaendelea kushirikiana kwa karibu na Mahakama katika kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati, kwa usawa na bila upendeleo.

Kwa upande wake, Naibu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama anayeshughulikia Maadili, Bi. Alesia Mbuya, alisema kuwa tangu ziara ya Jaji Mkuu Mstaafu Prof. Juma Ibrahim kufanyika mkoani Shinyanga mwezi Novemba 2022, Tume imeendelea kushirikiana kwa karibu na Kamati za Maadili ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Alibainisha kuwa ziara hiyo ililenga kukutana na watumishi wa Mahakama, Kamati za Maadili pamoja na wadau wa mnyororo wa haki, kwa lengo la kubadilishana mawazo na uzoefu kama njia mojawapo ya kudumisha ushirikiano.

Bi. Mbuya aliongeza kuwa Tume imekuwa ikiendesha mafunzo na uratibu wa karibu kwa Wajumbe wa Kamati hizo ili kuhakikisha maadili ndani ya Mahakama yanadumishwa kwa kiwango cha juu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO KAZI CHA MMMAM CHAFANYIKA SHINYANGA, KUWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA MALEZI NA MAKUZI BORA KWA MTOTO

    August 20, 2025
  • WAMILIKI WA VITUO VYA KULELEA WATOTO MCHANA SHINYANGA WAASWA KUSAJILI VITUO VYAO ILI KUTOA HUDUMA SALAMA KWA WATOTO

    August 20, 2025
  • RC MBONI MHITA ATETA NA MANAIBU WAZIRI KUHUSU AJALI YA MGODI WA NYANDOLWA – ATANGAZA MAENDELEO YA ZOEZI LA UOKOAJI

    August 19, 2025
  • RC MBONI MHITA APONGEZA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA KWA KUIMARISHA MAADILI NA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI.

    August 19, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa