• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AWAFARIJI WAFANYABIASHARA WALIOUNGULIWA MADUKA KAHAMA.

Posted on: October 26th, 2025

Na Johnson James, Kahama

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amewafariji wafanyabiashara waliopoteza mali zao kufuatia janga la moto lililotokea usiku wa kuamkia octoba 26, katika Mtaa wa Igalilimi, Kata ya Kahama Mjini, na kuahidi kuwa Serikali ya Mkoa itashirikiana nao katika kipindi hiki kigumu kwao.

Akiwa ameambatana na viongozi wa kamati ya Usalama na baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Manispaa Kahama, Mhe. Mhita leo Octoba 26. 2025 alitembelea eneo la tukio ambapo moto huo uliteketeza maduka sita kati ya 13 yaliyoko katika jengo hilo.

“Nawapa pole sana kwa hasara hii kubwa. Najua mmeathirika kiuchumi na kisaikolojia, lakini niwahakikishie kuwa Serikali ipo pamoja nanyi,” alisema Mhe. Mhita.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wafanyabiashara wote mkoani Shinyanga umuhimu wa kujikinga na majanga ya moto kwa kufunga vitambuzi vya moto (smoke detectors) na kuwa na vifaa vya kuzimia moto katika kila jengo la biashara.

Kwa upande wake, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Shinyanga, ASF Fatma Sato, alisema moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme katika moja ya maduka, na ulienea kwa haraka kutokana na bidhaa zinazowaka kwa urahisi kama magodoro, vitambaa na nguo.

Amesema kikosi chake, kwa kushirikiana na wananchi pamoja na kikosi cha zimamoto cha Mgodi wa Barrick Buzwagi, walifanikiwa kudhibiti moto huo , jambo lililosaidia kuokoa maduka saba yasiteketee.

Mmiliki wa jengo, Bi. Febronia Ikombe, alishukuru ujio wa Mkuu wa Mkoa na akaahidi kutekeleza agizo la kufunga vifaa vya tahadhari ya moto.

Mmoja wa wafanyabiashara, Bw. Paul Hamka, alisema ujio wa Mkuu wa Mkoa umewapa faraja kubwa na motisha ya kuanza upya.

Moto huo haukusababisha vifo wala majeruhi, lakini ulibainisha umuhimu wa tahadhari katika maeneo ya biashara.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA

    November 13, 2025
  • RC MHITA AKUTANA NA MSANII BANDO MC, APONGEZA JUHUDI ZA KUSAIDIA VIJANA SHINYANGA

    November 11, 2025
  • RC MHITA APONGEZA UONGOZI MPYA WA KANISA LA WASABATO NGBF MKOANI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • WANAFUNZI 29,193 KUFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KIDATO CHA PILI SHINYANGA.

    November 07, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA AWAHAMASISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI MKOANI SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKUU WA MKOA, MKOA WA SHINYANGA, 04 MTAA WA BOMA

    Anuani: P.O.Box 320, 37180,SHINYANGA, TANZANIA

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa