• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MHITA AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA KUTOKA JKCI KUTOA HUDUMA MAALUM KWA WANANCHI SHINYANGA

Posted on: August 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, leo Agosti 18, 2025 amewapokea rasmi madaktari bingwa tisa kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) waliofika mkoani hapa kwa ajili ya kutoa huduma maalum za afya kwa wananchi. 

Zoezi la kuwapokea madaktari hao limefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, likihudhuriwa na viongozi wa sekta ya afya mkoani hapa pamoja na wawakilishi wa wataalamu wa JKCI.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, Mhe. Mhita amesema ujio wa madaktari hao ni hatua kubwa katika kuboresha huduma za afya mkoani hapa na kusaidia wananchi kupata matibabu ya kibingwa bila kulazimika kusafiri kwenda jijini Dar es Salaam.

"Tunawakaribisha kwa moyo wa shukrani madaktari wetu bingwa. Huduma hizi ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wetu, hasa wenye matatizo ya moyo na kina mama wanaohitaji uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi," amesema Mhita.

Huduma zitakazotolewa katika kambi hiyo itakayofanyika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo zoezi ambalo linaenda sambamba na uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi  kwa kina mama. ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuimarisha afya za wananchi kwa kuwafuata walipo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge wamesisitiza kuwa kambi hiyo ni sehemu ya mkakati wa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kuimarisha ustawi wa jamii kupitia huduma jumuishi.

Kambi hiyo inatarajiwa kufanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kwa muda wa siku tano ikianza Agosti 18 hadi 22, 2025, ambapo wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi kufaidika na huduma hizo muhimu.

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AFISA UTAMADUNI MKUU AHITIMISHA SIKU YA NNE YA TAMASHA LA UTAMADUNI UKUNE, APONGEZA JUHUDI ZA KUHIFADHI MILA NA DESTURI ZA KISUKUMA.

    August 23, 2025
  • WAZIRI LUKUVI ATEMBELEA MGODI WA NYANDOLWA, AFIKISHA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

    August 22, 2025
  • MSANII MBOSSO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA OFISINI KWAKE.

    August 22, 2025
  • RC MHITA ATAKA KASI KUONGEZWA KWA UTOAJI VITAMBULISHO VYA WAFANYA BIASHARA,ARUHUSU SOKO LA IBINZAMATA KUTUMIKA KAMA GULIO.

    August 22, 2025
  • Angalia zote

Video

RC MHITA ALIVYOTOA KIBALI CHA KUTUMIKA KWA SOKO LA IBINZAMATA KUWA GULIO.... ASISITIZA ...
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa