• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AFIKA HANANG' KUWAFARIJI NA KUKABIDHI MISAADA YA KIBINADAMU

Posted on: December 22nd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amekabidhi misaada ya kibinadamu ikiwemo chakula, nguo na vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na wananchi wa Shinyanga kwa waathirika wa mafuriko ya tope yaliyoambatana na mawe kutoka Mlima Hanang' katika wilaya ya Hanang' Mkoani Manyara na kuwaomba kuendelea kumshukuru, kumuomba na kumtanguliza Mwenyezi Mungu kwa kila jambo.

RC Mndeme ameyasema haya leo tarehe 22 Des, 2023 wakati wa kukabidhi misaada kiwa kwa Mkuu wa wilaya ya Hanang Mhe. Janeth Mayanja ambapo pamoja na pole kwa wana Hanang' lakini pia alitoa pole kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tukio hili lililoathiri mali na kupelekea vifo.

"Msaada tunaotoa ni mdogo ukilinganisha na madhara yaliyotokea, hivyo tunaomba hiki kilichotolewa na wanashinyanga mkipokee," RC Mndeme.

"Shinyanga ni sehemu ya watanzania, tuliposikia janga hili tulipokea kwa masikitiko makubwa sana, kwa mapenzi mema waliyonayo wanashinyanga wakaona nao wamuunge mkono Mhe.  Dkt. Samia Suluhu Hassan na pia wawaunge mkono wananchi wenzao kwa kutoa pole kwa wanaHanang hivyo tumefika hapa katika mji huu wa Katesh kuwasilisha kwako mhe. DC pole zetu ili kuonesha umoja na kwamba tuko pamoja katika kipindi hiki kigumu ambapo kwa wenzetu wa Hanang wanapitia," amesema Mhe. Mndeme.

Kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Shinyanga ambao wamejitolea kutoa pole zao kwa ndugu zao wa Hanang, RC Mndeme amekakibidhi mifuko 1000 ya saruji, mchele kilo 700, unga wa mahindi kilo 355, unga lishe kilo 250, juisi za matunda mbalimbali katoni 500, chumvi pakti 90, sukari kilo 25, sabuni katoni 13, mafuta ya kupikia lita 5, viatu jozi 43, Belo za nguo 30 kati ya  hizi 27 ni nguo za wanaume na belo 3 nguo mchanganyiko.

Kwa upande wake DC Wilaya ya Hanang Mhe. Janeth Mayanja amemshukuru RC Mndeme kwa niaba ya wanashinyanga wote kwa ,huruma, utu, upendo, ubinadamu na undugu wa kweli waliouonesha kwa wanaHanang na kwamba msaada huu ni sehemu ya kumuunga mkono kwa vitendo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kadhia hii iliyowakumba wanahanang'.


HABARI PICHA

RC Mndeme wa pili kutoka kulia, akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi wa kwanza kulia, akifuatiwa na DC wa Katesh aliyesimama kushoto akifuatiwa na DC Mboni Mhita wa Kahama

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI MKOANI SHINYANGA WEKENI UMUHIMU KWENYE BIMA - DC. MTATIRO

    February 24, 2025
  • RC MACHA AKUTANA NA WAJUMBE WA BODI YA JTI WAKIONGOZWA NA MWENYEKITI WAKE BI. ANNE MAKINDA,

    February 21, 2025
  • RAS. CP HAMDUNI AFUNGUA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA SEKRETARIETI YA MKOA WA SHINYANGA

    February 21, 2025
  • TJMEANZA KUFANYIA KAZI MAELEKEZO YA MHE. WAZIRI MKUU - PROF. MBARAWA.

    February 20, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa