• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AFUNGUA KIKAO CHA TATHIMINI YA LISHE MKOA WA SHINYAGA

Posted on: August 9th, 2023

Na. Shinyanga RS.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme leo tarehe 9 Agosti, 2023 amefungua kikao cha tathimini ya lishe Mkoa wa Shinyanga ambapo pamoja na maelekezo mengine lakini pia ameziagiza Halmashauri zote Mkoani Shinyanga kutilia mkazo wa siku ya usafi kitaifa ambapo kila jumamosi ya kila mwisho wa mwezi huadhimishwa kwa kufanya usafi huku akiwataka kuwa wanaitangaza siku hiyo kwa kwa kuwakumbusha wananchi waweze kushiriki kikamilifu.

Mhe. Mndeme ameyasema hayo mbele ya wajumbe wa lishe mkoa ambao walipata wasaa wa kuwasilisha taarifa kutoka katika kila Wilaya zao ambapo kwa ujumla ilionesha tathimini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ni nzuri sana kwakuwa zimekuwa na alama nzuri zote.

"Leo tupo hapa kwa ajili kufanya kikao cha tathimini ya mkataba wa lishe mkoani kwetu ambapo kwa ujumla hali ipo vizuri sana, lakini jambo moja muhimu sana la kuzingatia ni kuwekea mkazo siku ya usafi wa mazingira ambapo kila jumamosi ya mwisho wa mwezi wananchi washirikishwe kufanya usafi kwa dhati kabisa na wawe wanakumbushwa kwa matangazo,"  alisema Mhe. Mndeme.

Kando na hayo, Mhe. Mndeme alisisitiza juu ya kutengwa kwa Tzs. 1000 kwa kila mtoto ambapo itatekelezwa kwenye afua za lishe jambo ambalo litaimatisha zaidi afya zao.

Aidha alielekeza Vijiji na Mitaaa yote Mkoani Shinyanga kufanya Maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ili elimu iweze kuwafikia wananchi wote, pia Halmashauri zote hapa Shinyanga zitumie vikao vyote vya kikanuni kuweka ajenda ya lishe ili iweze kujadiliwa ambapo watafanya tathimini ya wapi wamefikia na wapi wamekwama waweze kuboresha na kisha akawaagiza Afisa Lishe wote ndani ya Mkoa wa Shinyanga waende kwa wananchi kutoa elimu kupitia mikutano ya hadhara wasikae ofisini.

"Katika hili, naelekeza afisa lishe wote kwenda kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo yao ambapo mtafanya mikutano na hapo ndiyo mtaweza kutoa elimu kwa wananchi wetu, msikae ofisini nendeni kwa wanananchi mkaifanye kazi hii naagiza," alisisitiza Mhe. Mndeme

Katika hatua nyingine Mhe. Mndeme amewapongeza sana waandishi wa habari wote Mkoani Shinyanga kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhabarisha na kutoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na nje ya mkoa pia, jambo ambalo limepelekea jamii kuelimika sana na hivyo kusaidia kuimarisha afya zao, usafi wa mazingira na kupendezesha miji sambamba na kuelimisha umma juu ya kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya awamu ya sita kwa wananchi wake.

PICHA NA MATUKIO BAADA YA KIKAO 

Picha ikionesha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mndeme akikabishi zawadi kwa mshindi wa usafi na utunzaji wa mazingira kwa Halmashauri 6 za mkoa ambapo Manispaa ya Shinyanga waliibuka mshindi namba moja





@ortamisemi @christinamndeme18

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa