• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
    • eVibali |
Shinyanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Yetu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
      • Afya
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Shinyanga
    • Wilaya ya Kahama
    • Wilaya ya Kishapu
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu
    • Halmashauri ya Mji wa Kahama
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu
    • Halmashauri ya Wilaya ya Msalala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Bandari Kavu
  • Huduma
    • Kutoa Ushauri wa Kitaalam
    • Kutafsiri Sheria na Sera
    • Kuratibu Shughuli za Wadau
    • Ulinzi na Usalama
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Tafiti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

RC MNDEME AIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA KUFANYA VIZURI KATIKA NYANJA MBALIMBALI ZA MIRADI, USAFI WA MAZINGIRA, HATI SAFI MAIKA MITANO MFULULIZO NA KUVUKA LENGO LA MAKUSANYO KWA 102%

Posted on: June 24th, 2023

Na. Shinyanga RS

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme amehudhuria na kushiriki katika Kikao Maalumu cha Baraza kwa ajili ya kupokea na kujadili mapendekezo ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mkoa wa Shinyanga katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ikiwa ndiyo mwisho wa vikao hivi maalumu katika Mkoa wetu wa Shinyanga.

Katika kikao hiki Mhe. Mndme amewapongeza sana kwa kupata Hati Safi kwa miaka 5 mfululizo, kuongoza kwa ukusanyaji mapato mwaka wa 2021/2022 kwa asilimia 125, kuongoza kwa usafi wa mazingira Kitaifa, kutekeleza miradi mikubwa mingi ya kimkakati kwa kutumia mapato ya ndani, kuwa wa kwanza Kitaifa kwa masuala ya Utawala Bora na kufikia tarehe 23 Juni, 2023 Manispaa hii ilikuwa imekusanya asilimia 103 ikiwa imevuka lengo kabla ya kufika mwisho wa mwaka wa fedha 30 Juni, 2023 hakika wanastahili KUPEWA MAUA YAO.

“Kutoka ndani ya moyo wangu, nawapongeza sana Manispaa ya Shinyanga kwa kufanya vizuri  katika nyanja mbalimbali kama zilzivyotajwa hapo juu, kwakweli ninyi ndiyo sura na taswira ya Mkoa wa Shinyanga na katika hili mmetuheshimisha sana Mkoa kupitia aliyekuwa Mkurugenzi wenu Ndg. Satura na sasa mnae Mwl. Kagunze hakika Manispaa ya Shinyanga mnastahili kupewa MAUA YENU,” alisema Mhe. Mndeme.

Pamoja napongeza hizi, lakini aliwaelekeza mambo kadhaa yafanyike ikiwamo na kuhakikisha kuwa Machinjio ya Ndembezi panakuwepo na Rejista ya kuonesha idadi ya mifugo inayoingia kuchinjwa na inayokuwepo eneo hilo kusubiria wakati wa kuchinjwa, ushuru wa huduma uwe unakusanywa kwa kufuata na kutumia taarifa za TRA.

Maelekezo mengine ni kuwa, kuanzia sasa Kitengo cha Sheria kihakikishe kinafuatilia wadaiwa wote katika Kampuni ili walipe kwa wakati na wakishindwa kulipa kwa wakati basi Kitengo kiwapeleke mahakamani, makusanyo kwa njia ya Mashine yapelekwe Benki ndani ya masaa 24 tangu kukusanywa kwake, watenge moja kati ya vikao vya mwezi au robo ili kujadili hoja badala ya kusubiria mkaguzi, kulipa madeni yote likiwamo na deni la PSSSF pamoja na kuimarisha vyanzo vya mapato huku akimpongeza sana Satura.

“Kama alivyotangulia kupongezwa Jomaary Mrisho Satura (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, nami nimempongeza sana kwa namna ambavyo alikuwa mchapa kazi, alivyokuwa akishirikiana na (CCM) Serikali, Waheshimiwa Madiwani, Menejimenti, watumishina wadau wa maendeleo jambo ambalo liliwezesha Manispaa kufanya vizuri.

 

Aidha nimempongeza kwa kuendelea kuaminiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan @samia_suluhu_hassan kuendelea kumsaidia kazi katika Jiji la Dar es salaam, na pia nimemkaribisha Mwl. Alexius Kagunze Mkurugenzi mpya wa Manispaa,” alisema Mhe. Mndeme.

Picha ikimuonesha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias R. Masumbuko akielezea jambo wakati wa kikao cha CAG katika Ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo Manispaa ya Shinyanga.

Picha ikiwaonesha baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakiwa katika Baraza Maalumu kujadili taarifa ya CAG

Picha ikimuoesha Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Mwl. Alexius Kagunze wakati wa kikao cha CAG

 

 

Matangazo

  • No records found
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% LIPENI KWA WAKATI ILI PIA VIKOPESHWE NA VIKUNDI VINGINE - RC MACHA

    February 13, 2025
  • CP. HAMDUNI AKUTANA NA KAMATI YA MICHEZO YA JWTZ

    February 13, 2025
  • WANANCHI, LIPENI KODI YA ARDHI KWA WAKATI MUEPUKE RIBA - LEO KOMBA

    February 12, 2025
  • WAJUMBE WA BODI, TUMIENI TAALUMA ZENU KUISAIDIA HOSPITALI KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI- RAS CP. HAMDUNI.

    February 11, 2025
  • Angalia zote

Video

MIFUKO BANDIA ZAIDI YA ELFU 20 YAKAMATWA SHINYANGA
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Hotuba Mbalimbali
  • Video Mbalimbali
  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Picha za Matukio
  • Miongozo na kanuni

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Mfumo wa kutuma, kupokea na kufuatilia malalamiko, mapendekezo, maulizo na pongezi
  • Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Boma Street, Mwanza Road

    Anuani: P.O.Box 320, Shinyanga

    Simu: +255 28 2762222

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras@shinyanga.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2018. Mkoa wa Shinyanga. Haki zote zimehifadhiwa